Thursday, July 3, 2014

Wanalambalamba, Azam fc watahimili kasi ya Yanga, Simba na Mbeya City ili kutetea ubingwa wao msimu ujao?

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Julai 3, 2014, saa 3:00 asubuhi

MABINGWA wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wanatarajia kuweka kambi nje ya nchi kwa lengo la kujiimarisha zaidi kabla ya kuanza harakati za kutetea ubingwa wao pamoja na kucheza ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani.

Jemedari Said, meneja wa Azam fc amesema wamepokea mialiko kadha wa kadha, lakini wanasubiri kocha mkuu,  Mcameroon, Joseph Marius Omog achague wapi atakwenda.

“Ratiba ya kwenda nje ya nchi ipo. Kuna mialiko kadha wa kadha. Mwalimu baada ya kufanya maandalizi ya hapa nyumbani, yeye ndiye atachagua wapi pa kwenda. Yeye atachagua ni wapi anaona akienda timu itafanya maandalizi mazuri na kushiriki vizuri katika michuano ya CAF na ligi kuu”. Alisema Jemeadari.

10417523_774363632603995_9069252492513294123_n
Azam fc wameshaanza mawindo ya msimu mpya chini ya kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog.

Jemedari aliongeza kuwa walipozungumza na mwalimu alisema hatapeleka timu sehemu yoyote kwa ajili ya kujifurahisha bali atapeleka timu ambapo itapata uzoefu wa ligi ya mabingwa na itakuwa ni faida pia kwa ligi ya nyumbani.

Meneja huyo alisema kama mwalimu wao ataamua kuipeleka timu sehemu ilipokuwa msimu uliopita na kutwaa ubingwa kwa maana ya Afrika kusini hilo ni juu yake na kama ataamua kwenda sehemu nyingine, pia ni maamuzi yake.


Hata hivyo kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Azam wanatarajia kuweka kambi nchini Kenya au Amerika, lakini uongozi haujasema lolote zaidi ya kumsubiri Omog achague sehemu ya kuweka chimbo lake.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video