Friday, June 27, 2014



 http://ptblog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2014/06/ndumbalo1.jpg
Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi wa Simba sc,
Wakili, Dkt. Damas Ndumbaro Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 27, 2014, saa 3:49 alasiri

WEKUNDU wa Msimbazi Simba wanatarajia kumpata rais mpya, makamu wa rais na wajumbe wapya wa kamati ya utendaji katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo unaotarajia kufanyika juni 29 mwaka huu.
Awali uchaguzi huo uligubikwa na mizengwe hususani baada ya kuenguliwa kwa jina la mgombea wa Urais, Michael Richard Wambura.
Wambura alikata rufani mara ya kwanza katika kamati ya rufani ya uchaguzi wa TFF baada ya kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya mwenyekiti wake, Wakili,  Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kuliengua jina lake kwenye mchakato wa uchaguzi.
Sababu kubwa zilizosababisha Wambura kuenguliwa ni kuipeleka Simba mahakamani na kusimamishwa uanachama mwaka 2010.
Baada ya kamati ya rufani chini ya Jaji Julius Mutabazi Lugaziya kubaini Simba walifanya makosa kwa kumuacha Wambura akishiriki shughuli za Simba ikiwemo kulipia ada wakati walitangaza kumsimamisha, iliamua kumrejesha.
Kamati ya uchaguzi ya Simba ikaliengua jina la Wambura kwa mara ya pili baada ya kubainika kuongea maneno ya kampeni kabla ya muda, lakini `kidume` alikata rufani tena na akachinjwa rasmi na kamati ya rufani ya uchaguzi baada ya kubaini alifanya makosa.
 http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/05/Wanachama-Simba1.jpg
Wanachama wa Simba huu ndio muda wa kuijenga klabu yenu kwa kupata viongozi bora

Baada ya mizengwe ya muda mrefu sasa mambo yameiva ambapo leo hii kamati ya Uchaguzi ya Simba SC imesema kuwa inapenda kuwaalika wanachama wote wa Simba katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Klabu uliopangwa kufanyika Keshokutwa Jumapili, Juni 29 mwaka huu, katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na katibu mkuu wa Simba sc, Ezekiel Kamwaga, shughuli za uhakiki wa wanachama zitaanza saa moja kamili asubuhi na Mkutano umepangwa kuanza saa tatu kamili asubuhi na wanachama na wagombea wote wanaombwa kuwa wamekaa katika viti vyao kufikia muda huo.
Kamwaga alifafanua kuwa katika uchaguzi huo, jumla ya wagombea 27 wanatarajiwa kushiriki na Kamati ya Uchaguzi imeazimia kwamba suala la muda litazingatiwa sana safari hii kutokana na ukweli wa kuwepo kwa wagombea wengi.
“Ni matumaini ya Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC kwamba wanachama watazingatia muda wa kufika ili kurahisisha shughuli za kamati”.Ilisema Taarifa ya Kamwaga.
“Kamati inatangaza pia kwamba katika uchaguzi huo, ulinzi utakuwa wa kiwango cha juu; ingawa ina matumaini kwamba wanachama wote watakuwa watulivu ili kulinda jina, heshima na hadhi ya Simba SC.
Benki ya Posta”
Kamwaga aliongeza kuwa kwamba kwenye uchaguzi kutakuwa pia na huduma ya kutoa kadi kwa washabiki wa Simba wanaotaka kuingia katika mfumo mpya wa Benki ya Posta.
Simba na Benki ya Posta zimeingia katika makubaliano ya kutengeneza kadi hizo ambazo kwa utaratibu utakaotangazwa katika siku zijazo, ndiyo zitatumika kwa wanachama wote.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video