Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa Maximillian
Luhanga (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari jana kuhusu ziara yao
itakayofanyika katika mikoa yote baada ya mfungo wa Mwezi wa Ramadhan,
kustoto ni rapa wa bendi hiyo Raja Ladha (Na Mpiga Picha Wetu)
………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
BENDI ya muziki wa dansi nchini
Mashujaa, inatarajia kufanya ziara katika mikoa ya nchini nzima kwa
ajili ya kutoa shukrani kwa mashabiki wao waliowapigia kura kwenye tuzo
za Kilimanjaro Music Awards.
Akizungumza Dar es Salaam jana,
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa bendi hiyo Maximillian Luhanga, alisema
kuwa wamepata mafanikio makubwa kwa miaka miwili baada ya kupata tuzo
nane.
Alisema kuwa mwaka jana walipata tuzo tano na mwaka huu wamefanikiwa kupata tuzo tatu kutokana na kura za mashabiki wao.
Alisema kuwa wamejifunza mambo mengi katika muziki kutokana na kuwa wanakubali ushauri kutoka kwa mashabiki wao.
“Tunatarajia kufanya ziara
katika mikoa yote ya Tanzania baada ya kupata tuzo tatu mwaka huu na
hivyo hiyo ziara itakuwa kwa ajili ya kuwashukuru mashabiki wetu,”
alisema.
Alisema kuwa wamesharekodi
nyimbo mbili mpya ambazo watazitumia mikoani ikiwa ni kama zawadi kwa
mashabiki wao, ambapo nyimbo hizo ni Usidharau Sifuri na Kiu ya Haki.
Alisema kuwa ili waendelee kuwa
karibu na mashabiki wao kila mwezi watakuwa wanatengeneza matukio
mbalimbali ya bendi katika mitandao ya Kijamii.


0 comments:
Post a Comment