
Bata batani: Samir Nasri akipozi katika picha na demu wake, Anara Atanes, mjini Dubai baada ya mechi ya kirafiki ya Manchester City.
SAMIR
Nasri haendi kombe la dunia, lakini haimzuii kula bata batani na demu
wake wala kumharibia msimu ujao wa ligi kuu soka nchini England.
Kocha
wa Ufaransa Didier Deschamps alimtema kiungo huyo wa timu ya
Manchester City katika kikosi chake kinachotarajia kwenda kushiriki
kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Kitendo
cha Nasri kutemwa kilimkasirisha mno demu wake na kuporomosha matusi ya
nguoni kwa nchi ya Ufaransa na kocha mkuu wa timu ya taifa.

Maji ya moto: Didier Deschamps amemfungulia kesi Atanes baada ya kumtukana matusi ya nguoni

Atastaafu? Nasri anatafakari hatima yake ya soka la kimataifa baada ya kuachwa katika kikosi cha kombe la dunia
Licha ya maamuzi ya Deschamps kumuacha Nasri, nyota huyo mwenye miaka 26 ameonekana kutokuwa na wasiwasi na ameweka picha kwenye mtandao wake wa Twita akiwa na demu wake Anara Atanes nchini Dubai.
Man City walicheza mechi ya kirafiki baada ya kumaliza msimu dhidi ya Al Ain alhamisi iliyopita.
Atanes alimtukana kocha wa Ufaransa `mitusi` mikubwa mno, akisema:
a 's*** manager' for not picking Nasri. Hatukuona haja ya kutasfiri ili kupunguza makali.
Baada ya matusi hayo, Deshamps alimfungulia kesi mahakamani mwana mitindo huyo.
Wakati huo huo, winga wa Manchester United na timu ya taifa ya Ureno, Luis Nani yuko mapumzikoni na familia yake nchini Dubai kabla ya kujiunga na kikosi cha Ureno kwa ajili ya maandalizi ya kombe la dunia.
Nani ni miongoni mwa wachezaji 23 wa Ureno waliotajwa leo jumatatu kwa ajili ya safari ya Brazil

Nani akiwa na familia yake baada ya kutajwa katika kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya kombe la dunia
0 comments:
Post a Comment