
Mechi
ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Morocco
kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Zimbabwe iliyochezwa Jumapili katika Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 63,345,000.
Mapato
hayo katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Taifa Stars kuibuka na ushindi wa bao
1-0 yametokana na washabiki 11,079 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo kwa
viingilio vya sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 20,000.
Mgawo
wa mapato hayo ni asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni
sh. 9,662,796.61, gharama za kuchapa tiketi sh. 6,000,000, asilimia 15 ya
uwanja ni sh. 7,152,330.51, asilimia 20 ya gharama za mchezo sh. 9,536,440.68
na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu
Afrika (CAF) kwa pamoja wamepata sh. 30,993,432.20.

0 comments:
Post a Comment