Wednesday, March 19, 2014

 Na Baraka Mpenja , Dar es salaam


0712461976 au 0764302954


KIKOSI cha wagonga nyundo wa Mbeya, klabu ya Mbeya City kimeondoka leo asubuhi jijini Mbeya kuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kujiandaa mapema na mchezo wake dhidi ya Ruvu JKT machi 22 mwaka huu  uwanja wa Azam Complex, Chamazi.


Kwa mujibu wa Afisa habari wa klabu hiyo, Freddy Jackson  wachezaji wote wapo katika hali nzuri tayari kwa mchezo huo isipokuwa mchezaji Richard Peter ambaye ataukosa mchezo kwasababau hali yake haijatengamaa baada ya kuumia katika mechi yao dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora uwanja wa sokoine siku za karibuni.


Imeelezwa kuwa Peter bado  ana maumivu ya kawaida katika mbavu zake.


“Maandalizi yetu ni mazuri sana. Tumejiandaa kikamilifu,  tupo kamili kuzinyakua pointi tatu. Nayasema haya kutoka kwa kocha Juma Mwambusi”.


“Kocha anasema kikosi chake kina uwezo mkubwa sana wa kuibuka na ushindi katika mchezo huo”. Alisema Jackson katika taarifa yake asubuhi hii.


Kwa niaba ya club, Jackson  aliweka wazi  kuwa watakuwa makini sana na mchezo huu maana wamekuwa wakioneshwa michezo mibaya sana , hasa kwa hizi timu za majeshi wanapokutana nazo.


“Mfano mzuri ni mchezo wetu dhidi ya Rhino Rangers,  wachezaji wetu waliumizwa kwa makusudi kabisa. Pia tutakuwa makini zaidi na maamuzi ya marefa. Tunaomba mwamuzi atakaechezesha mchezo huo kuzingatia kanuni na sheria uwanjani ili kutoa haki kwa pande zote mbili”. Alisema Jackson.


Aidha aliwaomba mashabiki wao kuendelea  kuwaamini maana bado wanayo nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa.


Mbeya City  wapo nafasi ya tatu katika msimamo  wa ligi kuu soka Tanzania bara wakiwa na pointi 39, sawa na Yanga waliopo nafasi ya pili kwa pointi 39, lakini tafouti yao ni mabao ya kufunga na kufungwa.



Mpaka sasa Mbeya City wameshuka dimbani mara 21, wakati Yanga wao wamecheza mechi 18.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video