Friday, March 14, 2014

 Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
0712461976 au 0764302956

WAKIWA na machungu ya kutolewa katika michuano ya kimataifa, mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Young Africans, kesho watahamishia hasira zao kwa Mtibwa Sugar katika mechi ya ligi kuu uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Yanga wataingia kwa nguvu zote ili kupunguza maumivu waliyopata huko Alexndria nchini Misri kufuatia kutupwa nje ya ligi ya mabingwa barani Afrika na Al Alhy ya Misri kwa penati 4-3.

 Mchezo wa kesho unatazamiwa kuwa mgumu sana kutokana na mazingira ya timu zote mbili.

Mtibwa Sugar wanahitaji ushindi ili kusogea mbele katika msimamo kwani mpaka sasa wapo nafasi ya 8 wakiwa na pointi 25 ambapo wameshuka dimbani mara 20.

Msimu huu wana TamTam hao chini ya kocha Mecky Mexime hajawa na makali ya kutosha, hivyo kesho wataingia uwanjani kutafuta ushindi mbele ya mabingwa watetezi, ili angalau kujisogeza mbele.

Kwa upande wa Yanga wanahitaji kurejea kileleni mwa ligi kuu soka Tanzania bara kwani mpaka sasa wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 38, huku juu yake akiwepo Mbeya City pointi 39 na kileleni wapo Azam fc wenye pointi 40.

Faida kwa Yanga ni kwamba wamecheza mechi 17 mpaka sasa, wakati Mbeya City wameshuka dimbani mara 21, na Azam fc amecheza mechi 18 mpaka sasa.

Pia Yanga  wana kikosi bora kuliko Mtibwa Sugar, hivyo wanapewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi, lakini imekuwa ngumu sana kwa wakata miwa kukubali kipigo kutoka kwa timu kubwa za Simba na Yanga.

Mashabiki wa Yanga wanahitaji kuona kiwango cha klabu hiyo kilichooneshwa kwenye mechi mbili zilizopita dhidi ya Al Ahly.

Yanga ilicheza mpira mkubwa sana katika mchezo wa machi mosi jijini Dar es saalam na mechi ya marudiano nchini Misri ambapo walifungwa bao 1-0 ndani ya muda wa kawaida na kutolewa kwa penati 4-3 kufuatia wastani wa mabao kuwa 1-1 ukizingatia Yanga nao walishinda bao 1-0 uwanja wa Taifa.

Nao vinara wa ligi kuu, Azam fc watakuwa na kibarua dhidi ya wagosi wa Kaya katika dimba la Azam complex, Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Endapo Azam fc wenye pointi 40 watapoteza mchezo na Yanga watashinda, basi wanajangwani watarejea kileleni.

Lakini kama Azam fc itashinda na Yanga itashinda, basi Azam fc wataendelea kubarizi kileleni kama kawaida kwani Yanga atakuwa na pointi 41 na Azam fc pointi 43.

Kama  Yanga atafungwa kesho, na Azam akafungwa, msimamo utabaki kama ulivyo sasa. Azam watakuwa kileleni kwa pointi 40, Mbeya City nafasi ya pili pointi 39 na Yanga nafasi ya tatu pointi 38.

Endapo Yanga atatoka sare kesho na Azam atashinda, maana yake, Mbeya City ataporomoka kwa nafasi moja kutoka ya pili kwenda ya tatu kwakuwa Yanga ana wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa japokuwa pointi zitafungana.

Kwa mazingira hayo, mechi za kesho ni ngumu sana kwa Yanga na Azam fc kutokana na ubora wa Mtibwa Sugar na Coastal Union.


Tayari Yanga wapo Morogoro na wachezaji waliosafiri ni;

Walinda Mlango: Deo Munish "Dida", Juma Kaseja na All Mustafa "Barthez"

Walinzi: Juma Abdul, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, David Luhende, Nadir Haroub "Cannavaro", Kelvin Yondani na Ibrahim Job

Viungo: Frank Domayo, Athumani Idd "Chuji",  Nizar Khalfani, Hassan Dilunga na Haruna Niyonzima


Washambuliaji: Saimon Msuva, Said Bahanuzi, Hamis Kizza, Emmanuel Okwi, Didier Kavumbagu, Hussein Javu na Jerson Tegete

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video