Wednesday, March 19, 2014

 Nahodha wa Azam fc, John Raphael Bocco `Adebayor na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub `Canavaro`wakiwekana sawa ili kujua nani anaanzia kushambulia wapi. Bocco hakufunga leo hivyo kushindwa kuendeleza rekodi yake ya kuzifunga timu kubwa
 Hawafungiki: Kikosi cha Azam fc leo hii kilicheza vizuri zaidi baada ya kuwa pungufu kufuatia kadi nyekundu ya Erasto Nyoni kwa kutoa lugha chafu kwa mwamuzi.
 Kikosi cha Yanga leo hii kimepoteza penati baada ya Hamis Kiiza kukosa, lakini walipata nafasi kadhaa za kufunga, ila hawakuweza kuzitumia
Kocha msaidizi wa Azam fc,  Kalimangonga Ongala (wa kwanza kulia) alisema safari ya ubingwa bado ni ndefu kwao. Wapili kutoka kulia ni kocha mkuu, Mcameroon, Joseph Marius Omog akifuatilia mchezo wa leo.
 Kocha mkuu wa Yanga, Hans Van Der Pluijm (wa kwanza kulia) alisema wamecheza vizuri na kupoteza nafasi, lakini wanao muda wa kujisahihisha na kutetea ubingwa wao.
 Mashabiki hawakuamini kama kweli wamebanwa na Azam fc
Nao mashabiki wa Azam fc walikuwa hawaamini kama kweli watafungwa, lakini wakashuhudia Kevin Friday akiwakomboa dakika ya 83 baada ya kufunga bao la kusawazisha

 Shughuli ilikuwa pevu, Azam fc walicheza kwa kujituma zaidi licha ya kuwa pungufu
 Nahodha wa Yanga sc, Nadir Haroub `Canavaro` tangu aoneshe soka kubwa dhidi ya Al Ahly anawavutia zaidi mashabiki wa Yanga na kusahau maneno yao ya nyuma kwamba amezeeka
 Komaa mwana tuokoe kona: Kaseja akimpa maarifa mwenzake.
 Ana bahati Mbaya : Juma Kaseja alitunguliwa na Kevin Friday, hakika bao limeibua minong`ono tena.
Hapa wachezaji wa Yanga wapo makini kuzuia mpira wa kona. Hadi Hamis Kiiza baada ya kukosa penati ikabidi arudi kuzuia ili balaa lisitokee

Picha zote na Baraka Mpenja
.............................................................................
Na Baraka Mpenja Dar es salaam


0712461976 au 0764302956

AZAM FC wamefanikiwa kulinda rekodi yao ya kutofungwa msimu huu kufuatia bao la kusawazisha la dakika za lala salama kupitia kwa kinda wake, Kevin Friday dakika ya 83  na kulazimisha sare ya 1-1 dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Dar Young Africans, Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kinda huyo aliyepandishwa kutoka kikosi cha pili aliitumia vyema pasi ya kiungo fundi, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na kumchambua kipa mkongwe Juma Kaseja na kushangilia kwa hisia kali kuashiria yeye ndiye mkombozi wa Azam fc.

Yanga walikuwa wa kwanza kuandika bao katika dakika ya 14 kupitia kwa Mrundi, Didier Kavumbagu aliyekutana na mpira uliorudi baada ya kupanguliwa na kipa Aishi Salum Manula baada ya kutokea piga ni kupige langoni mwa Azam. 

Kwa matokeo ya leo, Azam fc wamefikisha pointi 44 kileleni, huku Yanga wakiendelea kusalia nafasi ya pili kwa pointi 40.

Hata hivyo Azam fc wamecheza mechi 20, wakati Yanga leo ilikuwa mechi ya 19.

Bahati ya Yanga ilionekana kuendelea kuwepo baada ya kupata penalti dakika ya 69 kufuatia beki Said Mourad kuunawa mpira uliopigwa na Didier Kavumbangu, lakini  Hamisi Kiiza ‘Diego’ alidakiwa penati hiyo kwa ustadi mkubwa na mlinda Mlango,  Aishi Salum Manula .

Dakika 20 za mwisho, Azam fc walipata pengo la mchezaji mmoja kufuatia beki wake wa kulia Erasto Edward Nyoni kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa madai ya  kutoka lugha chafu kwa mwamuzi.

Licha ya kadi hiyo, Azam fc waliendelea kucheza kwa kujituma zaidi wakijua wamejeruhiwa, na jitihada zao zikasababisha sare ya bao 1-1.

Kwa ujumla mchezo ulikuwa mkali na kuonesha ubora wa vikosi vya timu zote mbili.

Baada ya mechi hiyo, kocha msaidizi wa Azam fc, Kalimangonga Ongala alisema safari ya ubingwa bado ni ndefu kwasababu ushindani ni mkubwa.

“Tchetche alifunga bao lilikataliwa. Kadi nyekundu ya Erasto sijui kwanini alitolewa,  kwasababu alitamka kuwa Mungu ndiye anayejua. Sasa kuna tatizo gani hapo?”. Alihoji Kalimangonga.

Aidha, aliwapongeza vijana wake kwa kucheza soka zuri baada ya kadi nyekundu.

“Ulikuwa mchezo mgumu kwetu. Wachezaji kuna wakati hawakuwa watulivu. Lakini baada ya kuwa pungufu wamecheza soka la juu sana. Tunawapongeza kwa ukomavu wao”. Alisema Kalimangonga.

Kocha huyo aliongeza kuwa sasa hesabu zao ni kuelekea mchezo ujao dhidi ya JKT Oljoro katika uwanja wao wa Azam complex.

Naye kocha wa Yanga, Mholanza, Hans Van Der Pluijm alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri, walipata nafasi hawajazitumia, hivyo kulazimisha sare.

“Ulikuwa mchezo muhimu kwetu. Bado tuna muda wa kujiboresha na kutetea ubingwa wetu. Najua matokeo ya leo sio mazuri kwetu, lakini tunatakiwa kujipanga zaidi”. Alisema Pluijm.

Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Juma Kaseja, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Frank Domayo, Simon Msuva, Hassan Dilunga, Didier Kavumbangu/Mrisho Ngassa dk73, Hamisi Kiiza/Hussein Javu dk87 na Emmanuel Okwi.
Azam FC; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gadiel Michael, Said Mourad, Kipre Balou, Himid Mao, Salum Abubakar, John Bocco, Kipre Tchetche na Khamis Mcha/Kevin Friday dk49.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video