Thursday, November 7, 2013


1 
Mratibu wa Dawati la Magonjwa ya Milipuko na Maafa kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Grace Saguti akiwasilisha mada kuhusu Sheria na Kanuni za Kimataifa za Afya kwenye semina ya wanahabari  jijini Dar es Salaam. 2 
Mtaalamu wa Masuala ya Epidemiolojia Dk. Vida Mmbaga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akiwasilisha mada kwenye semina hiyo.
Hussein Makame, MAELEZO
SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) limeitaka sekta binafsi kushikiana na Serikali kutoa taarifa za magonjwa ya milipuko ili kukabiliana na athari za magonjwa hayo ndani na nje ya nchi.
Hayo yamesemwa na Mratibu wa Dawati la Magonjwa ya Milipuko na Maafa kutoka WHO, Dk. Grace Saguti wakati akiwasilisha mada juu ya Sheria za Kimataifa za Afya kwenye semina ya wanahabari iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Alisema kuwa kwa sasa dunia inakabiliwa na changamoto ya magonjwa mbalimbali ya milipuko inayoenezwa kutoka ndani ya nchi na nje na kuathiri jamii ya Watanzania lakini hayaripotiwi mapema ili kuyadhibiti.
Dk. Saguti pia amewataka wananchi kutoa taarifa za magonjwa ya milipuko pindi tu wanapoona dalili za magonjwa hayo ili kuyadhibiti na kuepusha madhara yanayoweza kuenea katika sehemu kubwa ya jamii.
Kwa upande wake Dk. Vida Mmbaga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii alisema kuwa watu 10 walifariki dunia mkoani Rukwa kwa ugonjwa wa uti wa mgongo kwa kipindi cha mwezi Oktoba mwaka huu.
Alisema katika kipindi hicho wengine 34 waliugua ugonjwa huo ingawa hadi sasa ni mgonjwa mmoja tu ndiye anayeugua ugonjwa huo huku baada ya Serikali kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuwahi hospitali.
“Hatua nyingi iliyochukuliwa ji kuelimisha jamii juu ya namna ya kudhibiti na kuzuia ugonjwa huo, pia tulizuia mikusanyiko ya watu kwenye jamii, kutoa matibabu na kushirikisha sekta mbalimbali katika kudhibiti ugonjwa huo” alisema Dk. Mmbaga.
 Aliwashauri wananchi kuepuka misongomano yenywe watu wengi na iwapo mtu atagundulika na dalili za ugonjwa huo akuwahi mapema kwenye vituo vinavyotoa huduma ya afya ili kupata dhibiti ugonjwa husika.
Alisema dalili kubwa za ugonjwa huo ni kukakamaa kwa shingo, homa kali, kuumwa kichwa, na kutapika  na kwamba asilimia 5 hadi 10 ya wagonjwa wanaougua uti wa mgongo hufariki ndani ya saa ya siku moja au mbili.
Dk. Mmbaga aliwataka watu wanaobaini kupata dalili hizo kwenye hospitali au vituo vya afya na kuwatahadharisha ndugu wa mgonjwa kutomtenga mgonjwa kutokana na kuugua ugonjwa huo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video