Waziri
Mkuu Mizengo Pinda amesema ziara ya ujumbe wa watu zaidi ya 70 kutoka
Serikali za Mitaa nchini China utasaidia kukuza uchumi wa Tanzania
na kuendeleza ushirikiano baina ya nchi hizo hadi kwa manufaa ya
wananchi.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akifungua
majadiliano hayo kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu
Julius .K. Nyerere jijini Dares Salaam.
“Ziara
hii itasaidia kujenga uwezo kwa kusimamia shughuli za Serikali za Mitaa
kwa pamoja kuboresha ushirikiano ,kukuza uchumi na ushirikiano wa
kibiashara na maendeleo ya sekta binafsi kupitia fursa za biashara,
uwekezaji na viwanda kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizi mbili.
Alisema
Tanzania kio tayari kufanya kazi kwa pamoja na ujumbe huo, hivyo
aliwataka viongozi mbalimbali wa Serikali za Mitaa nchini kutumia
fursa kwa kubuni maeneo ya uwekezaji.
Kwa
upande wake Kiongozi wa msafara huo, Naibu Gavana wa Jimbo la Shandong
, Xia Geng, aliyataja maeneo ya ushirikiano kupitia ziara hiyo ni ,
shughuliza kiuchumi, biashara, nishati na huhifadhi wa mazingira.
Naye
Balozi wa China nchini, Lu Youqing alisema serikali ina nafasi ya
kutengeza ajira kwa wananchi, hivyo aliishauri viongozi wa Serikali za
Mitaa nchini kuliangalia suala hilo.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali(TAMISEMI),
Hawa Ghasia alisema alitembelea China mwaka jana akiwa na timu yake
ambapo wamejifunza kuwa , wana maendeleo mazuri katika masuala ya
serikali za mitaa.
Aliongeza
kuwa maendeleo hayo yamewafanya kutotegemea vyanzo vya fedha kutoka
Serikali Kuu wala rasilimali watu, inapanga,inaogeza na kutumia vyanzo
vyake vya mapato kwa usimamizi mdogo wa Serikali na kukopa fedha kutoka
taasisi mbalimbali za kifedha.
Waziri huyo alisema pia inahusishisha jamii katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo
Ujumbe
wa watu wapatao 70 kutoka Serikali za Mitaa kutoka China, wakiwemo
magavana,mameya na wafanyabiashara ambao umekuwepo kwa ziara ya siku
nne kwa ajili ya majadiliano hayo na mawaziri wa Sekta mbalimbali,
wakuu wa Mikoa, wakuu wa Wilaya, makatibu Tawala wa Mikoa.
Wengine
ni baadhi ya Mameya/Wenyeviti wa Halmashauri za Jiji, Manispaa, Miji na
Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri,Taasisi za Serikali na
Binafsi pamoja na Wafanyabiashara.


0 comments:
Post a Comment