Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
WAKATA
miwa wa mashamba ya Manungu Turiani Mkoani Morogoro, wenyewe wanaita
Mji kasoro bahari, wana TamTam Mtibwa Sugar kuanza mawindo yao ya
mzunguko wa pili desemba 10 mwaka huu.
Mwenyekiti
wa klabu hiyo, Jamal Bayser amesema mipango imekaa sawa na ifikapo siku
hiyo wachezaji wote watatakiwa kuripoti mazoezini ili kuendelea
kujiimarisha zaidi kabla ya kuanza ngwe ya lala salama.
“Mipango
yetu ni kuhakikisha tunafanya vizuri, na ndio maana tutaanza tarehe za
mapema ili kumpa muda wa kutosha kocha wetu, mecky Mexime kusuka kikosi
chake ili kuwa na nguvu zaidi za kusaka nafasi nzuri”. Alisema Bayser.
Bayser alisema kwa mujibu wa mapendekezo ya kocha wao, hawatakiwa kusajili mchezaji yeyote kwani kikosi kina nyota wa kutosha.
“Mwalimu
alisema wachezaji alionao wanamtosha, hivyo nasisi hatujasajili kabisa
katika dirisha hili dogo, lakini uhakika ni kuwa Mtibwa inao wachezaji
wengi na wazuri. Ikumbukwe sisi tumekuwa tukizalisha wachezaji wazuri
kwa wakati wote wa ushiriki wa ligi kuu”. Alisema Bayser.
Akizungumzia
kuondoka kwa Issa Juma Awadh aliyejiunga na Simba SC katika dirisha
dogo la usajili, Bayser amesema hawana shida kwani mara nyingi timu
kubwa zimekuwa zikiwanasa nyota wao, lakini bado wanaendelea kutengeneza
wengine wazuri zaidi.
“Sisi
Mtibwa sio watu wa kukurupuka, tuna utulivu mkubwa inapofika wakati wa
usajili, matunda yanaonekana na ndio maana hawa wanaojiita wakongwe wa
soka la Tanzania wanakodolea macho kwetu”.Alisema.
Mtibwa
Sugar waliwahi kuwa mabingwa mara mbili mfululizo wa ligi kuu, mwaka
1999 na 2000, lakini miaka ya karibuni wamekuwa washiriki zaidi kwani
wanashindwa hata kuingia nafasi tatu za juu licha ya historia yao nzuri
katika michuano hii ya ligi kuu soka Tanzania bara.


0 comments:
Post a Comment