Friday, November 29, 2013

Mboga aina ya Biringanya ikiwa shambani tayari kwa kuanza kuvunwa. Picha na Maktaba 
…………………………………………………………………………
Katika siku za karibuni Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika iliwahakikishia wakulima kwa mara nyingine tena kwamba Rais Jakaya Kikwete ametoa kauli ambayo inawaruhusu wakulima kuwa huru katika kuuza mazao yao iwe kwa soko la ndani au nje.
Kauli hiyo imetolewa na msemaji wa wizara hiyo Richard Kasuga wakati akizungumza na gazeti hili.
“Kwa sasa wakulima wameruhusiwa kuuza bidhaa zao kwa namna wanavyotaka katika soko wanalotaka ili mradi wafuate sheria,” alisema Kasuga.
Wakulima hao wamesema kwamba wao ndiyo wanaochangia asilimia 95 za gharama za kilimo inakuwaje sasa wakati wakivuna Serikali ndiyo iwapangie wapi pa kuuza.
“Wakulima wanachangia asilimia 95 ya gharama za kilimo ….hakuna anayewasaidia kuanzia hatua za awali za kukodi shamba, kuliandaa, kulima , kupanda, kuondoa magugu na kuvuna. Wanafanya bila msaada lakini cha ajabu Serikali inawapangia soko, hii si sawasawa.”
Kauli imetolewa na mmoja wa maofisa wa Chama cha Wafanyabiashara, wenye viwanda na kilimo Peter Lanya wakati akizungumza na Mwananchi kwenye mahojiano.
Lanya ambaye ni Makamu Mwenyekiti (kilimo) na pia Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji Bidhaa nje (Tanzania Exporters Association) amesema kwamba wakulima ni vyema wakaruhusiwa kuuza bidhaa zao mahali ambapo watapata maslahi zaidi.
Alisema kwa wakulima kazi yao hiyo ndiyo inayowaingizia kipato ambacho hukitumia kwa ajili ya familia na hivyo kuwanyima nafasi ya kupata kipato kizuri si sahihi.
“Ni jambo la kustaajabisha kuwalazimisha wakulima ambao tegemeo lao la pekee la kuwapatia kipato ni kilimo kuuza bidhaa zao katika soko ambalo halina maslahi kwao. Nadhani ni vyema kuwaacha huru kutafuta masoko yenye maslahi,” alisema Lanya.
Kama wakulima hawataruhusiwa kuuza kwa namna wanayoona wao inafaa, kwa vyovyote watashindwa kuwa na kipato cha kuwasaidia kila siku na kudunduliza fedha zinazotakiwa kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo.
“Kama wasipopata fedha za kutosha kwa ajili ya matumizi ya msingi ya kwao wenyewe kama matibabu hawatakuwa na uwezo wa kufanya shughuli za kilimo kwa msimu unaofuata na hivyo kuongeza kasi ya umaskini,” alisema Lanya.
Hata hivyo alionya wageni wanaofika nchini na kununua mazao yakiwa bado shambani kabla ya msimu wa mavuno.
“Wakati Serikali inafanya kila liwezekanalo kuleta maendeleo ya kiuchumi , ni vyema ikawa ya kwanza kuzuia wageni ambao hununua bidhaa zikiwa bado shambani, kabla ya muda wa mavuno,” alisema.
Kama Serikali itachukua hatua hiyo ya kuzuia wageni itasaidia wakulima kuwa na mavuno ya kutosha na kujihakikishia hali bora kwao binafsi na kwa taifa.
Kwa mujibu wa Lanya, kama Serikali inataka kuwa na uhakika wa usalama wa chakula ni vyema ikawasaidia wakulima kupata pembejeo ili wakulima hao wafanye kazi yao ya kulima kwa gharama nafuu.
Alisema ni dhahiri kwa kuboresha uzalishaji wa mazao utasaidia kuchangia kukua kwa pato la ndani (GDP).
“Kwa kuwa chakula hakipo katika biashara na hivyo kuonesha kuwa mchango wake GDP ni mdogo,wakulima wakiwezeshwa na kuwa na pembejeo,zana husika na utaalamu ni dhahiri kwamba kipato cha GDP kitaboreshwa zaidi,” anasema Lanya.
Mawazo hayo ya Lanya yameungwa mkono na mwenyekiti na mwanzilishi wa Chama cha Wahitimu wa Kilimo Chuo Kikuu cha Sokoine Stephano Kingazi ambaye alisema kuwazuia wakulima kuuza mazao yao soko la nje si kitu chema hata kidogo.
Alisema kuondolewa kwa ushindani katika kilimo kunasababisha bidhaa kuwa na bei chini na matokeo yake mkulima kuendelea kuwa maskini.
Hata hivyo alisema kwamba ipo haja kwa Serikali ya Tanzania kushawishi wananchi kutambua umuhimu wa kuwa na akiba ya chakula.
Alisema ni vyema kanuni zikawekwa kusaidia kuhakikisha kwamba kuna akiba ya chakula nchini.
Aidha Serikali inatakiwa kutambua kwamba ili kuboresha hali ya upatikanaji wa chakula nchini ni lazima kuwapatia wakulima mbegu bora. “Ukiangalia sasa utaona kwamba mbegu nyingi zilizopo sokoni ni mbaya kuliko zile ambazo wananchi wamezoea kuzitumia, Serikali lazima kuhakikisha wakulima wanapata mbegu bora ili kuongeza tija” alisema Dk Kingazi.
Dk Kingazi alishauri Serikali kutumia kila uwezekano kuhakikisha kwamba wakulima wanakwenda sambamba na teknolojia mpya ya kilimo.
Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Richard Kasuga pamoja na Rais Kikwete kuruhusu wakulima kuuza bidhaa zao katika soko wanalotaka, Serikali imechukua hatua kuboresha uzalishaji wa mazao ya chakula.
“Serikali inawekeza kwenye miundombinu ya umwagiliaji ambapo wakulima wanaweza kutumia, kupatikana kwa mbegu bora na kuwapatia pembejeo katika bei wanayoweza kuimudu.”
Hata hivyo msemaji huyo amekiri kwamba Serikali bado ina upungufu wa maofisa ugani.
CHANZO: MWANANCHI

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video