Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
MAAFANDE
wa jeshi la kujenga Taifa kutoka wa mkoani Pwani, Ruvu Shooting Stars
wameendelea wamesisitiza nia yao ya kuongeza nyota kadhaa ili kuimarisha
kikosi chao kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu soka
Tanzania bara mwezi januari mwakani.
Kocha
Mkuu wa klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa `Masta` amezungumza na
mtandao huu na kueleza kuwa mpaka sasa hawezi kusema anamsajili nani,
lakini mchakato unaendelea na muda wowote atatoa taarifa kwa vyombo vya
habari.
“Nilishawasilisha
mapendekezo yangu, viongozi wapo hatua za mwisho kulishughulikia suala
hili. Lazima niongeze nguvu sehemu ya Mlinda Mlango na ushambuliaji
kwani mzunguko wa kwanza tuliruhusu mabao mengi na kukoasa nafasi nyingi
za wazi, hii inaashiria kuwa maeneo hayo kuna udhaifu”. Alisema Mkwasa.
Mkwasa
aliongeza kuwa wanatakiwa kufanyia kazi pia sehemu ya kiungo hasa baada
ta kuondoka kwa nyota wao kinda Hassan Dilunga aliyetimkia kwa mabingwa
watetezi na vinara wa ligi hiyo, Dar Young Africans.
Kocha
huyo alisema mzunguko wa pili utakuwa mgumu sana kwani kila timu
inajiwinda, lakini atafanya kila linalowezekana kuwa na kikosi bora cha
kuhimili vishindo vya wapinzani.
“Nipo
katika wakati wa mpito kusuka kikosi changu, tuna madhaifu kadhaa,
lakini nitayarekebisha ili kuendana na kasi ya ligi kuu mzunguko wa
pili”. Aliongeza Mkwasa.
Msimu
uliopita Ruvu shooting ilimwagiwa sifa nyingi wa wapenda soka nchini
kwa kuonesha kiwango kizuri sana, lakini msimu wa mwaka huu wanaonekana
kuwa na makosa mengi hasa sehemu ya ulinzi na ushambuliaji.


0 comments:
Post a Comment