Mkurugenzi
wa Sera na Mipango Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bibi
Joyce Mwakisyala akisisitiza jambo wakati akiongea na Wadau mbalimbali
wa Michezo katika ukumbi wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Wadau wa
Michezo wamekutana leo Jijini Dae es Salaam na Wizara kwa ajili ya
kujadili, kutoa maoni, ushauri na mapendekezo kuhusu Rasimu ya Mkakati
wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka 2013.
Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo, Bibi. Juliana
Yassoda.
Mwakilishi
wa Katibu Mkuu Shirikisho la Ngumi la Taifa (BFT), Bw. Michael
Changarawe akichangia hoja wakati Wadau wa Michezo walipokutana katika
Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo kwa
ajili ya kujadili, kutoa maoni na ushauri kuhusu Rasimu ya Mkakati wa
Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka 2013 leo
Jijini Dar es Salaam.
Bibi.
Sharifa Luvindi (aliyesimama) wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika
Idara ya Sera na Mipango akichangia katika mjadala kuhusu Rasimu ya
Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Michezo ya Mwaka
2013 uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
(Picha zote na Concilia Niyibitanga, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.)

0 comments:
Post a Comment