Monday, November 25, 2013

Mkuu wa Mkoa akiwa amekaa juu ya dawati lililotengenezwa na wananchi  wa Kata ya Nenkwa Tarafa ya Inyonga kwa kutumia nguvu zao ikiwa ni kuunga mkono serikali kuondoa tatizo hilo ili watoto wasiendelee kuka chini. MZEE WA KIMILA AKIMZAWADIA RC MBUZI 
Mzee wa Kabila la kipimbwe mkazi wa kijiji cha Mamba  ambaye jina halikufahamika mara mmoja  akimzawadia Mkuu wa Mkoa Mbuzi Mnyama ikiwa ni Ishara ya upendo kwake kwa kuonesha furaha kufika kuwatembelea kijiji kwao na kuhimiza shughuli za maendeleo SAM_5458 
Mkuu wa MKOA WA KATAVI DKT Rajabu Rutengwe akikagua ujenzi wa mnada katika kijiji cha majimoto na kukuta umejengwa chini ya kiwango na kuagiza mradi huo urudiwe tena
(Picha Na Kibada Kibada Katavi)

Na Kibada Kibada -Katavi
Serikali Mkoani Katavi imepiga marufuku watu kuishi kwenye maeneo yasiyoruhusiwa na kuwataka waondoke mara moja ama sivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria iwapo watakaidi.
Hatua hiyo imekuja siku chache kupita baada ya kuondolewa wale wote waliokuwa wakiishi maeneo ya hifadhi ya wanyama pori ya taifa ya Katavi na kwenye maeneo ya vyanzo maji huku wakifuga na wengine kuendesha shughuli za kijamii kama kulima na shughuli nyingine.
Watu hao wote wametakiwa kuondoka kwa kuwa walikuwa wamekwishaondolewa kufuatia operation tokomeza ujangili iliyofanyika mwezi oktoba mwaka na kuwaondoa wengine wameanza kurudi katika maeneo hayo.
Kufuatia kuwepo kwa tetesi kuwa wapo baadhi ya wananchi hususani wafugaji kuanza kurejea katika maeneo hayo wakiwa na makundi yao ya mifugo,  Mkuu wa Mkoa ametoa agizo la kuondoka haraka katika maeneo hayo na kusisitiza kuwa wasidanganywe na wanasheria uchwala kuwa watawatete pindi watakauwa wamevunja sheria hizo.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alipata nafasi ya kutembelea baadhi ya maeneo yaliyoondolewa wananchi na wengine wameanza kurejea na kukutana na makundi ya mifugo na kuagiza waondoke.
Akiwa katika moja ya mikutano yake ya hadhara katika maeneo mbalimbali alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa Tarafa ya Mamba Wilayani Mlele wa Vijiji vya Kata za Ikuba, Mede, Majimoto Usevya na Mamba kuwa waliondolewa na kuchomewa nyumba zao wakati wa operation tokemeza ujangili ilipokuwa ikiendelea jambo ambalo walidai walionewa wakaomba kurudi kwenye maeneo hayo waliyoyaita yao.
Wananchi hao walieleza kuwa wao walikwenda kuishi huko kwa maelekezo waliyopewa na badhi ya viongozi wa serikali za vijiji kwa kuuziwa maeneo hayo ambayo baadhi yao yako ndani ya hifadhi ya wanyama na mengine yako kwenye vyanzo vya maji ambavyo vimeharibiwa kutoka na shughuli za kibinadamu kama kilimo ufugaji, ukataji miti, na nyinginezo ziliathiri kwa kiasi kikubwa maeneo hayo.
Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe ya operation tokomeza majangili iliyofanyika wilayani Mlele,  Mkuu wa Wilaya hiyo Kanali Ngemela Lubinga alieleza kuwa katika operation hiyo iliyoanza oktoba 14 mwaka huu kwa kujumuisha askari wa Jeshi la wananchi Tanzania( JWT) askari polisi,Usalama wa Taifa wataalamu toka Halamshauri na askari wa Hifadhi ya Rukwa /Lukwati jumla ya kaya 577 ziliondolewa ndani ya maeneo ya hifadhi ya Taifa ya Katavi,
Katika operation hiyo silaha tisa zikiwemo (SMG ) nne zilisalimishwa na nyingine 150 zilikamatwa zoezi hilo limesaidia sana majangili na waharibifu wa mazingira kudhibitiwa na maliasili ya nchi kulindwa kutokana na kuwepo kwa watu waliokuwa wakiharibu mazingira na maliasili za Taifa na wengine kuingiza mifugo katika Hifadhi za Taifa na maeneo tengefu.
Katika zoezi hilo la tokomeza ujangili kwa wilaya ya mlele maeneo yaliyoguswa ni Kata za Ilunde,Mapili,Ikuba,Ugalla,Sitalike,Mwamapuli,Mamba,Machimboni,na Itenka,kwa wananchi waliokuwa wakiishi ndani ya maeneo yasiyoruhisiwa na wengine ndani ya hifadhi na vyanzo vya maji.
Hivyo Mkuu wa Mkuoa amepiga marufuku kwa mtu yeyeote kuishi katika maeneo yaliyokatazwa na serikali badala yake waende katika maeneo yao ya vijiji waliyopimiwa na yanayotambulika kisheria, na kusisitiza kuwa wasidanganywe na wanasheria uchwala kuwa wakirudi katika maeneo hayo watawasaidia .
Naye Mkuu wa Wilaya Kanali Ngemela Lubinga amesisitiza kwa wananchi kuishi na kufuata sheria za nchi na kufuata maelekezo yanayotolewa na viongozi wao kuliko kuwa wajeuri kwani ujeuri hausaidii kitu, badala yake Utaumia, Nchi inatawaliwa kwa kufuata sheria kanuni na Taratibu zilizowekwa

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video