Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Raundi
ya 12 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imeendelea leo (Novemba 2 mwaka huu)
kwa mechi nne kuchezwa katika katika miji minne tofauti.
Azam
fc wana `Lambalamba` wamerejea tena kileleni leo hii na kuwashusha
Yanga waliokuwa wakiongoza kwa pointi 25 baada ya kupata ushindi wa
mabao 3-0 dhidi ya Ruvu Shooting, uwanja wa Azam Complex, Chamaz, Dar es
salaam na kukalia usukukani kwa kujikusanyia pointi 26 sawa na Mbeya
City ambao nao leo hii wameshinda bao 1-0 dhidi ya Ashanti United Uwanja
wa sokoine , Mbeya, lakini wanazidiana mabao ya kufunga na kufungwa.
Hadi
mapumziko, Azam FC walikuwa mbele kwa mabao 2-0 yaliyotiwa nyavuni
kupitia kwa Kipre Herman Tchetche katika dakika ya kwanza tu ya mchezo
baada ya kuwachomoka mabeki wa Ruvu Shooting na kinda Joseph Kimwaga
aliyepandishwa kutoka timu ya vijana msimu huu, alifunga bao lake katika
dakika ya 45 akiunganisha kichwa krosi iliyochongwa na beki , Waziri
Salum.
Kipindi
cha pili, Azam walianza soka kwa umakini mkubwa na uangalifu mkubwa na
dakika ya 70 Khamis Mcha `Vialli` alifunga bao la tatu kwa shuti kali
baada ya kumtoka beki wa Ruvu Shooting.
Kikosi
cha Azam FC leo: Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Said Mourad,
Aggrey Morris, Kipre Balou, Khamis Mcha, Himid Mao/Jabir Aziz dk58,
Kipre Tchetche, Humphrey Mieno na Joseph Kimwaga/Farid Mussa dk69.
Ruvu Shooting: Abdul Seif, Michael Pius, Stefano Mwasyika, Mangasini Mbonosi, Shaaban Suzan, Juma Dion, Juma Nade, Hassan Dilunga, Saidi Dilunga, Elias Maguri na Cossmas Lewis
Ruvu Shooting: Abdul Seif, Michael Pius, Stefano Mwasyika, Mangasini Mbonosi, Shaaban Suzan, Juma Dion, Juma Nade, Hassan Dilunga, Saidi Dilunga, Elias Maguri na Cossmas Lewis
Huko
Mbeya wenyeji wa uwanja wa Sokoine, Mbeya City wamejikusanyia pointi
tatu na kurejea nafasi ya pili katika msimamo baada ya ushinidi wa bao
1-0 dhidi ya wauza Mitumba wa Ilala, Ashanti United.
Bao
hilo limetokana na krosi iliyochongwa na beki wa kushoto wa Mbeya City,
Hassan Mwasapili katika dakika ya 30 na katika harakati za kuokoa
mchezaji wa Ashanti Samir said Ruhava alijifunga.
Hata
hivyo shuhuda wa mtandao huu pale jijini Mbeya, Laudens Simkonda
Galimoshi ameeleza kuwa, Mbeya City leo walibanwa sana na wameshindwa
kuonesha kasi yao mbele ya watoto wa mjiji.
Alisema
kuwa baada ya mchezo huo kocha mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi
amekiri timu yake kutocheza vizuri ingawa ameweka bayana kuwa mechi za
mfululizo zimeathiri kikosi chake.
Huko Uwanja wa Manungu Complex mkoani Morogoro, Mtibwa Sugar wameshinda bao 1-0 dhidi ya JKT Oljoro.
Bao pekee la Mtibwa Sugar limefungwa na Salim Mbonde na kuwapa raha mashabiki wa Mtibwa waliofurika katika uwanja huo.
Huko
dimba la CCM Mkwakwani jijini Tanga, Mgambo walioneshana kazi na
Coastal Union na mpaka dakika 90 zinamalizika timu hizo zimetoka suluhu
pacha ya bila kufungana.
Raundi
hiyo itakamilika kesho Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo
Tanzania Prisons itakuwa mwenyeji wa Oljoro kwenye Uwanja wa Kumbukumbu
ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi
za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7
mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashanti United vs
Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, na Ruvu Shooting vs Mtibwa
Sugar.
Novemba
7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa
Tanzania Prisons.
0 comments:
Post a Comment