Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
KIKOSI
cha Wakatalunya, Fc Barcelona kimewasili leo jijini Milani nchini
Italia tayari kwa kipute cha kesho cha kundi H katika michuano ya ligi
ya mabingwa barani Ulaya (UEFA) dhidi ya AC Milani jumanne ya kesho.
Barcelona
watakabliana na wenyeji wao katika dimba la San Siro na leo hii nyota
wake Neymar, Alex Song na Dani Alves walipiga picha moja kali wakiwa
katika mavazi ya suti safi kabisa baada ya kutua Italia.
Nyota
hao walivalia suti kali zilizobuniwa vizuri, miwani ya nguvu na
kusababisha wafanyakazi wa uwanja wa ndege kudhani kuwa waagizaji wa
filamu wamewasili.

Wakali: Neymar (kushoto), Dani Alves (katikati) na Alex Song (kulia) wakionekana watanashati wakubwa jijini Milani
Safari
ya Milan si ngeni kwa wachezaji wa Barcelona kwani timu hizo zimekutana
mara sita katika misimu miwili iliyopita na kwa kipindi chote hicho,
Barca wametawala zaidi na kuwatoa mara mbili AC Milani katika michunao
hiyo ya UEFA.
Jumanne
ya kesho usiku, miamba hiyo inakutana kusaka pointi tatu muhimu katika
kundi lao la H linalojumuisha mabingwa wa Scotland, klabu ya Celtic na
wachechemeaji wa Uholanzi, klabu ya Ajax.
Milan kwa sasa wana hali mbaya zaidi ligi ya Seria A baada ya kuanza vibaya na wapo nyuma kwa pointi 13 kwa vinara AS Roma.
Pia wanandinga hao wa Italia wanakabiliwa na wimbi la majeruhi ambapo
mlinda mlango wao Christian Abbiati, Mlinzi Daniele Bonera na
mshambuliaji Stephan El Shaarawy, Mario Balotelli na Giampaolo Pazzini
bado wanatibiwa katia chumba cha matibabu.

Wakali wawili: Alexis Sanchez (kushoto) na Jonathan dos Santos (kulia) -wakionesha mashati yao yaliyobuniwa vizuri

Kwenye pipa: Nyota wa Barcelona wakiwa katika pozi la picha ndani ya ndege wakielekea jijini Milan
0 comments:
Post a Comment