Viongozi
 hao wakiwa wakielekea kwenye ukumbi kwa ajili ya kushiriki hafla ya 
kumuaga aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na 
Michezo Bw. Seth Kamuhanda (katikati). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara 
hiyo Bi. Siaba Nkinga na kushoto ni Naibu wake Profesa Elisante Ole 
Gabriel.  
 
 
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa 
Elisante Ole Gabriel akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni 
rasmi wa hafla hiyo Bw. Seth Kamuhanda iliyofanyika jijini Dar es 
Salaam.  
Aliyekuwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth 
Kamuhanda akihutubia wakati wa hafla ya kuagwa kwake iliyofanyika leo 
jijini Dar es Salaam.  
 
Aliyekuwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth 
Kamuhanda akihutubia wakati wa hafla ya kuagwa kwake iliyofanyika leo 
jijini Dar es Salaam.  
 
Katibu
 Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Siaba Nkinga 
akimkabidhi zawadi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Seth 
Kamuhanda.  
 
 
Aliyekuwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth 
Kamuhanda (aliyesimama katikati) akiifurahia zawadi aliyopewa na Katibu 
Mkuu mpya wa Wizara hiyo katika hafla iliyoandaliwa na Wizara hiyo. 
Kushoto ni Katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo Bi. Siaba Nkinga na kulia ni 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel. Hafla 
hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam. 
 
 
Aliyekuwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth 
Kamuhanda (kushoto) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, 
Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel wakiangalia 
kwa furaha zawadi aliyokabidhiwa Bw. Kamuhanda kwenye hafla ya kuagwa 
kwake.  
 
 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akikabidhiwa zawadi.  
 
 
Aliyekuwa
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth 
Kamuhanda (wa tatu toka kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya 
pamoja na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na 
Michezo. 
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO, DAR ES SALAAM
Na Eleuteri Mangi.
WAMILIKI
  wa vyombo vya habari nchini wameaswa kuwajengea mazingira mazuri 
waandishi wa habari wa vyombo vyao ili waweze kuhabarisha umma wa 
Watanzania mambo mbalimbali yanayotokea ndani na nje ya nchi kwa 
kuzingatia weledi wa taaluma yao.
Rai
 hiyo imetolewa na Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake wa kuitumikia 
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Seith Kamuhanda jana 
alipokuwa anaagwa na watumishi wa wizara hiyo katika hafla iliyofanyika 
kwenye Uwanja wa Michezo wa Taifa jijini Dar es Salaam.
“
 Wamiliki wa vyombo vya habari wajenge mazingira mazuri ya kuwawezesha 
waandishi wa habari kusafiri ndani na hata nje ya nchi. Kwa kufanya 
hivyo unawapa fursa nzuri ya kujifunza mambo mengi ya kuihabarisha jamii
 ya Watanzania.
“Mwandishi
 asiye safari anakuwa na uelewa finyu wa mambo kwani ni jambo la msingi 
ajue nchi nyingine mambo yanaendaje ili aweze kulinganisha na maendeleo 
ya nchi yetu,” alisema Kamuhanda.
 Kamuhanda alisema kuwa wamiliki wa vyombo vya habari kuwapa fursa waandishi wa habari kusafiri  hilo ni jukumu lao la kwanza.
Kamuhanda
 aliongeza kuwa hata yeye alipokuwa mwandishi wa habari alijifunza mambo
 mengi alipokuwa akisafiri ndani na nje ya nchi, kwani kusafiri 
kunapanua mawazo na kuwa na uwezo mpana “exposure” wa kupambanua mambo 
juu ya nini cha kuandika na kuuhabarisha umma kulingana na maadili ya 
uandishi wa habari.
Aidha,
 Kamuhanda aliwaasa wamiliki na waadishi wa habari kuutumia vizuri uhuru
 wa vyombo vya habari uliopo hapa nchini. Sanjari na hilo, aliviasa vile
 vinavyokiuka miiko na maadili ya habari na kutumia vibaya uhuru huo 
vitambue kuwa wote wapo kwa ajili ya kuiletea sifa nzuri nchi yetu.
Kwa
 upande wake Katibu Mkuu wa sasa wa Wizara hiyo, Sihaba Nkinga 
amempongeza Katibu Mkuu huyo aliyemaliza muda wake kwa kuitumikia Wizara
 hiyo kwa uaminifu kwa   kipindi  cha  wa miaka minne.
Sihaba
 alisema kuwa Wizara anayoiongoza itaenzi kwa kusimamia na kuendeleza 
mambo aliyoanzisha Kamuhanda ikiwemo kudumisha umoja wa watumishi katika
 wizara na taasisi zake.
Naye
 Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni Profesa  Hermans Mwansoko akitoa neno 
la shukrani kwa Kamuhanda  kwa niaba ya wafanyakazi alisema wizara hiyo 
 itamkumbuka Kamuhanda kwa mpango wa kuwa na ofisi ya uhakika Dodoma, 
kuanzisha Bodi ya Filamu, kujali afya na uzima wa watumishi na kujali 
suala la jinsia katika ngazi za maamuzi ndani ya Wizara.
Kamuhanda
 alikuwa  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo  na kufanya kazi chini ya Mawaziri 
George Mkuchika, Naibu wake Joel Bendera, Dkt. Emmanuel Nchimbi, Naibu 
wake Fenella Mkangara.
Hadi
 mabadiliko ya nafasi za makatibu wakuu yalipotokea   hivi karibuni 
alifanya kazi chini ya Waziri Fenella Mkangara Naibu wake akiwa Amos 
Makala.


0 comments:
Post a Comment