Saturday, September 14, 2013


DC ASISITIZA JAMBOMkuu wa Wilaya ya Mpanda akiongea na Kamati ya Ulinzi na usalama juu ya operasheni ya kuwaondoa wahamiaji holela wanaoishi maeneo yasiyoruhusiwa wilayani Mpanda na kusababisha uharibifu wa mazingira  na kuchangia kukauka kwa maji ya Mto Katuma  unaotiririsha maji kupeleka katika Hifadhi ya Wanyama pori Katavi na wanyama aina ya Viboko kukosa maji hivyo kutambika na penginge kufa. WAJUMBEWajumbe wa Kamati ya ulinzi na usalama wakimsikiliza Mkuu Wilaya ya Mpanda akitangaza operation elimisha na ondoa makazi holela maeneo yasiyoruhusiwa Mpanda na Mkoa wa Katavi. AFISA 1Kaimu Afisa Maliasili na Mazingira Wilaya ya Mpanda Josephin Rupia akielezea mikakati ya uondoaji wahamiaji holelea katika maeneo yasiyoruhusiwa na okoa uharibifu wa mazingra.
 (Picha zote na Kibada Kibada Ofisi ya H/Wilaya ya Mpanda Katavi)
……………
Na Kibada Kibada –Mpanda Katavi
Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imetangaza oparasheni  maalum ya kuwaondoa wahamiaji holela waliovamia maeneo ya wazi ya mistu iliyotengwa na serikali kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira na kuharibu vyanzo vya maji ya Mto Katuma ambao ndio tegemeo la wakazi wa Mji wa Mpanda kupata maji  ambayo pia yanategemewa na wanyama walioko hifadhi ya Taifa ya Katavi.
Akizungumza ofisini  kwake  Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Mpanda ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima ameeleza kuwa operation hiyo ni kwa ajili ya kuokoa uharibifu wa Mazingira na Vyanzo vya maji hususani kuokoa uharibifu unaofanywa na watu waliovamia  maeneo ambayo hayaruhusiwi na kuweka makazi na kufanya shughuli zao za uzalishaji mali hali ambayo inachangia uharibifu mkubwa wa mazingira.
 Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa wageni wengi wanaoingia katika Wilaya ya Mpanda wameathiri  ardhi kutokana na mwingiliano wa wageni hao,sababu nyingine zinazochangia uharibifu huo  ni kuingia kwa mifugo kwa wingi bila kufuata utaratibu hivyo kuchangia uharibifu wa mazingira hasa wafugaji  na wakulima wanaolima kandokando ya mto Katuma ambao unategemewa na wananchi Mkoa wa Katavi hususani Wakazi wa Mji wa Mpanda  pamoja na  hifadhi ya Taifa ya wanyama pori  Katavi.
Hivyo kutokana na mwingiliano huo ambao umeathiri sana mbuga hiyo ya Katavi na wanyama kama viboko wanaoishi kwa kutegemea maji  wanatabika na wengine wanakufa kutokana na kukauka kwa maji ya  Mto Katuma ambao unamwaga maji yake katika Vijito vinavyotirirsha maji katika hifadhi hiyo ya Katavi.
Kutokana na hali hiyo ipo haja ya kupambana vya kutosha kulinda mto huo  na vyanzo vayke, hivyo inatakiwa kutoa elimu kwa wakulima na watu wanaolima ovyo kwenye vyanzo vya maji,na pili kuwaondoa  wale wote ambao hawaruhusiwi kuishi maeneo ambayo hayakurusiwa hivyo ni wahamiaji holela wanatakiwa wakakae kwenye vijiji vilivyopimwa.
Mkuu huyo wa Wilaya ameyataja maeneo yatakayohusika na operasheni hiyo itakayo anza Septemba 14,mwaka huu  kuwa ni Eneo la Kamama lililopo katika ya Makazi ya wakimbizi ya  Mishamo naKata ya Mpandandogo,eneo hili alieleza kuwa  ni eneo la wazi  kwa ajili ya matumizi ya Serikali.
Ameeleza kuwa   zipo hekta 46,000  zilizotengwa kwa ajili ya  shughuli  za Kiserikali ikiwemo shughuli za uwekezaji,pia limetengwa kwa ajili ya shughuli za vijana  wanaounda vikundi kwa kujiunga pamoja kwa ajili ya shughuliza kilimo na uzalishaji mali, pamoja na eneo lingine litakalotumika kwa ajili kwa kuweka Kambi ya Jeshi la kujenga Taifa JKT Mkoani humo ambalo uongozi wa Mkoa uliomba upatiwe eneo hilo.
Eneo la pili lililoathiriwa ni Mto Katuma ambalo limeathiriwa sana watu wanolima  hadi pembeni ya Mto,hivyo kuanzia Msimu ujao wananchi wameelimishwa  na kuellekezwa kuwa msimu wa kilimo ukifika watatakiwa walime kuanzia mita 60 kando ya Mto ili kulindamazingira nakuepuka  uharibifu  wa mazingira ili kuepuka kukausha maji ya Mto Katuma .
Akizungumzia operasheni hiyo ameleza kuwa nyingine itanza Septemba 20 mwaka huu kwa kuwapa elimu wananchi na  wanaolima na kuishi kandokando ya Mto Katuma kwa kuanza  na hatua ya kuwaelimisha kuhusiana na madhara ya uharibifu wa mazingira.
Pia kuwa ameleza itafuatia  na operation nyingine ya kuwahamisha wananchi wanaoishi  kwenye vilima vya Bugwe ambavyo ndiyo chanzo cha maji ya vijito vyote vinavyotiririsha na kumwaga maji katika mto katuma.
Ameleza kuwa    vyanzo vyote vya mto luega, Katuma na na mito mingine  vyanzo vyake vya maji  vinaanzia kwenye milima ya Bugwe kilipo kijiji cha Bugwe  na watu waliovamia bila utaratibu hasa kwenye milima ya Bugwe wanatakiwa kuondoka na kurudi kijijini wakati taratibu zinafanyika kuwaondoa na namna ya kukihamisha kijiji kwa kufuata taratibu kuhamisha.
 Suala la kijiji au kukifuta  Kijij hicho liko nchini ya ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) wanaenedelea kuwasiliana na kuona namna ya kufanya.
Pamoja na operasheni hiyo Mkuu wa Wilaya ameonya watakaohusika na operationi hiyo kuzingatia taratibu kanuni na sheria bila kukiuka utaratibu akaonya kuwa wafanye kazi kwa kufuata utaalamu na siyo kwa shuruti.
 Kwanza watoe elimu waweleze kwa nini wanataka kuwahamisha na pia washirikishe viongozi  wa serikali ya kijiji  Wataalam wa maeneo husika ili kuondoa migangano pamoja wanasiasa husika katika maeneo husika wala wasionee mtu.
Akasisitiza kuwa sheria izingatie utu,izingatie utaratibu na ufuatwe na siyo kuathiri wala kukiuka haki za binadamu.
“Twende kuelimisha kwanza na kuhamasisha”Naagiza mkafanye kazi kwa utaratibu siyo shuruti wapewe elimu kwanini wanahamishwa.”alisema Mkuu wa Wilaya.
Kwa Upande wake Kaimu Afisa Maliasili Mistu na Mazingira Josephin Rupia alieleza kuwa kabla ya kuamua kufanya operasheni hiyo wameisha toa elimu kwa wananchi na kutoa matangazo kuwa watu wanatakiwa kuondoka kwa hiali kurudi vijijini maeneo yaliyopimwa.
Amesema tayari viwanja zaidi ya miambili (200) kwa ajili ya makazi ya watu vimepimwa katika Kijiji cha Vikonge hivyo mahali pa kuishi wameisha tegewa hakuna haja kuendelea kuishi maeneo ambayo siyo rasmi na hayaruhusiwi

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video