
Miss
 Utalii Tanzania 2013, Hadija Mswaga, anaondoka nchini siku ya Jumanne 
Tarehe 1-10-2013 kuelekea Equatorial Guinea kuwakilisha Tanzania katika 
Mashindano ya Dunia ya Miss Tourism World 2013. Atasafiri kwa ndege ya 
shirika la ndege la Ethiopian Airline. 
Katika
 mshindano hayo yanayoshirikisha nchi 126 duniani kote, na kuoneshwa 
LIVE katika Televisheni Duniani kote, Miss Utalii Tanzania 2013, anabeba
 ujumbe wa kutangaza Hifadhi ya Ngorongoro Crater kama moja ya maajabu 
ya Dunia Afrika. 
Akitoa
 sababu za kuibeba Hifadhi ya ngorongoro katika mashindano hayo, Hadija 
Mswaga, alisema kuwa mbali ya hifadhi hiyo kuwa ni ya kipekee duniani, 
lakini ndiyo hifadhi ambayo chimbuko la binadamu wa kwanza kuishi 
duniani, pia hifadhi hiyo ndio kitovu cha hifadhi ya faru nchini, mbali 
ya kuwa ndiyo hifadhi pekee duniani ambako binadamu na wanyama wanaishi 
na kushirikiana maisha ya kila siku bila ya kudhuriana.
Wakati
 sasa umefika tena wakati sahihi kwa hifadhi ya ngorongoro kuwa hifadhi 
kiongozi kwa umaarufu ,pato la utalii na kutembelewa na watalii wengi 
zaidi duniani alisema hadija.

0 comments:
Post a Comment