Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Zitto Kabwe (Mb) akionesha Leseni mpya za Udereva mbele ya wajumbe wa kamati yake wakati kamati hiyo ilipokutana na Hazina kujadili namna bora ya kukusanya mapato ya Serikali hususani yale ya makosa ya barabarani kwa kutumia mfumo wa risiti za ki electroniki kwa kuwa leseni hizo zipo kwenye mfumo wa kisasa. Kamati hiyo imeileza Hazina jinsi fedha nyingi za makusanyo mbalimbali zinavyopotea kwa kutumia mfumo wa zamani wa risiti za kawaida na hata mara nyingine serikali kutofaidika na mapato hayo licha ya kwekeza zaidi katika mifumo hii. Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Zitto Kabwe (Mb) akikisitiza jambo kwa ujumbe kutoka Hazina wakati wa kikao cha kamati ya PAC na watendaji kutoka Hazina Naibu katibu Mkuu Hazina Bi. Elizabeth Nyambibo akijibu baadhi ya hoja zilizotolewa na wajumbe wa kamati ya Bunge ya PAC kujadili masalwa mbalimbali ya utendaji wa wizara hiyo walipokutana na kamati hiyo leo Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali LAAC Mhe.Rajaab Mbarouk Mohamed akiongoza kikao cha kamati hiyo leo ilipokutana kujadili Hesabu za Manispaa ya Arusha wakati wa Vikao vya Kamati vinavyoendelea Jijini Dar Es Salaam. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Seleman Zedi Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali LAAC Mhe.Rajaab Mbarouk Mohamed akiongoza kikao cha kamati hiyo leo ilipokutana kujadili Hesabu za Manispaa ya Arusha wakati wa Vikao vya Kamati vinavyoendelea Jijini Dar Es Salaam. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Seleman Zedi na Katibu wa Kamati hiyo Dickson Bisile Wajumbe wa Kamati ya LAAC wakifuatilia kikao kwa makini Mjumbe wa Kamati ya LAAC Mhe. Yusufu Nasir akiuliza swali kwa watendaji wa Manispaa ya Arusha wakati wa vikao vya Kamati ya Bunge ya LAAC jijini Dar leo.
0 comments:
Post a Comment