Wednesday, July 3, 2013

63
Kiungo Kinda, Omega Seme (pichani kushoto) anaelekea Tanzania Prisons kwa mkopo
Na Baraka Mpenja 
Viongozi wa maafande wa Tanzania Prisons ya jijini Mbeya maarufu kwa jina la “Wajelajela” wamekiri kumalizana na kiungo mahiri wa klabu ya Yanga ya Dar es salaam, Omega Seme ambaye anajiunga kwa mkopo na timu yake ya zamani.
Katibu mkuu wa wajelajela, Sadick Jumbe amewashukuru viongozi wa Yanga kuwaelewa na kuwaruhusu kumchukua mchezaji huyo, na julai 5 siku ya Ijumaa atakuwepo jijini  Mbeya kujiunga na wenzake.
Jumbe alisema msema kweli ni mpenzi wa mungu, Yanga wamewapa kwa mkopo na sio kwamba wamemnunua, kikubwa alisisitiza kuwa nyota huyo alianzia soka Prisons na sasa amerejea nyumbani ambapo wanaamini watafanya makubwa akiwepo kikosini.
“Omega ni kijana mzuri, anacheza vizuri sana. Anahimili sana safu ya kiungo, tumepata mkataba wake na tunajua atafanya vizuri sana akicheza namba nane”. Alisema Jumbe.
Pia katibu huyo alisema kinda huyo alikuwa miongoni mwa majina ambayo kocha wao mkuu Jumanne Chale alipendekeza, hivyo Yanga kuwapatia kijana huyo wanashukuru sana.
Kwa upande wake Omega seme, alisema mpaka sasa hawezi kusema lolote, lakini siku ya Ijumaa atazungumza na kuweka wazi suala lake.
“Kila kitu namaliza Ijumaa, unajua unapopelekwa kwa mkopo unaweza kukubali au kukataa”. Alisema Omega.
Akizungumzia kuondokewa na baadhi ya wachezaji wao akiwemo Sino Agostino aliyetimkia kunako klabu ya Msimbazi, kipa David Abdallah aliyehamia Mbeya City, Elias Maguli aliyejiunga na Ruvu Shooting, katibu huyo alisema wamepata nyota wapya walioziba nafasi za wachezaji hao.
“Tuna wachezaji wengi sana, Enock Nyanda, Madafa, Ibrahim saka na wengine wengi, wanaotosha kuziba nafasi zao”. Alisema Jumbe.
Pia alisisitiza kuwa msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara watakuwa fiti mno, watatoa upinzania mkubwa sana na kuwashangaza wanaojiita wafalme wa soka la Tanzania, Yanga na Simba.
Jumbe alisema jina la Prisons sio geni masikioni mwa watu, ni timu yenye historia ya kufanya vizuri sana, sasa timu ile iliyowakilisha taifa michuano ya kimataifa ipo njiani.
“Nimeweka muziki mkali, siku nitakayokuja kucheza na Simba au Yanga Dar es salaam, tafadhali mashabiki waje waone makali yetu, tutakufa na mtu”. Alisema Jumbe.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video