Monday, July 1, 2013

Na Baraka Mpenja
Mabingwa wa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Yanga ya Dar es salaam “kwalalumpa Malysia”  kesho wanaanza kupasha misuli yao moto kujiandaa na mitanange ya ligi kuu msimu wa 2013/2014 na michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
Afisa habari wa klabu hiyo Baraka Kizuguto amezungumza na MATUKIO DUNIANI na kubainisha kuwa Yanga wanaanza mazoezi na sio kambi hapo kesho maeneo ya Uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola,  iliyopo Mabibo, Dar es Salaam. 
 “Ni kweli kesho tunaanza mazoezi, kila kitu kinakwenda vizuri, na hapo kesho tunaanza mazoezi. Naomba tuongee vizuri na si kupotoshana taarifa, kesho Yanga inaanza mazoezi na sio kambi”. Alisema Kizuguto.
Kizuguto Alisema kwa siku kadhaa wachezaji watakuwa wakijifua na kurejea makwao, kabla ya kuingia kambini rasmi zikisalia wiki chache kabla ya kuanza kwa ligi.
Afisa habari huyo alisisitiza kuwa kesho mazoezi yanaanza saa mbili asubuhi ambapo kocha wao mkuu, Mholanzi ambaye anatarajia kuwasili leo kutoka kwao, Ernie Brandts ataongoza mazoezi hayo.
“Mwalimu atawasili leo na kesho atakuwepo mazoezini, kikubwa ni mashabiki wetu kuwa na imani kubwa na vijana wao”. Alisema Kizuguto.
Afisa habari huyo aliongeza kuwa wachezaji wote wanatambua juu ya kuanza mazoezi hayo, hivyo kesho mapema asubuhi watakuwepo uwanjani kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara.
Mabingwa hao ambao watakuwa wawakilishi pekee wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani, wanaendelea na zoezi la usajili pamoja na kuwaongezee mikataba baadhi ya wachezaji wao.
Leo hii taarifa za ndani kutoka katika klabu hiyo zinaeleza kuwa wachezaji nyota wa klabu hiyo Nizar Khalfan na Oscar Samwel Joshua wameongezewa mikataba ya miaka miwili.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video