Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
“Negredo, Sergio Aguero na Edin Dzeko ,Stevan Jovetic”. Washambuliaji hao wote wana viwango vya juu, sasa swali ni moja, nani kuwa chaguo namba moja kwa kocha mpya wa City, Manuel Pellegrini?.
Miamba ya soka nchini England na wenye jeuri ya pesa, klabu ya Manchester City imethibitisha kumsaini mshambuliaji hatari Stevan Jovetic kutoka Fiorentina kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 25.8 baada ya mwanandinga huyo wa kimataifa wa Montenegro kufuzu vipimo vya afya katika dimba maridhawa la Etihad.
Inaeleweka kuwa City watalipa kiasi cha Pauni Milioni 22.4 na ada itapanda kutokana na kukua kwa malipo ya posho ya nyota huyo mwenye uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu.
Pia Uhamisho wa nyota mwingine , Alvaro Negredo umethibitishwa, huku akikabidhiwa jezi namba tisa.
Kipaji cha kweli: Kufika kwa Stevan Jovetic kutaongeza makali ya safu ya ushambuliaji ya Manchester City
Uhamisho umekamilika: Alvaro Negredo amesainishwa na City na kupewa jezi namba tisa

Karibu Manchester: Mshambuliaji raia wa Montenegrin, Jovetic akiwasili katika Hoteli ya Manchester jana usiku
Mchezaji mwingine mpya kutoka Sevilla, Alvaro Negredo aliingia katika hoteli hiyo usiku wa jana
Mwaga wino hapa: Negredo akiwa na mkurugenzi wa michezo wa City , Txiki Begiristain (kushoto) na wakala wake wakati wa kusaini mkataba 
Haina noma, barida tu!: Nyota huyo atapambana kutafuta namba pamoja na Negredo, Sergio Aguero na Edin Dzeko

Tayari ametulia zake: Jovetic amewasili katika klabu mpya ya City na sasa kilichobaki ni kushindana kupata nafasi kikosi cha kwanza

0 comments:
Post a Comment