Mahmoud Ahmad Arusha
Waziri mkuu Pinda kukabidhi Madawa
 yenye thamani ya tsh.16.2 milion kwa Hospitali ya mkoa mount Meru 
wakati atakapowatembelea wagonjwa walipata majeruhi kwenye muendelezo 
uliotokea jana wa  mlipuko wa bomu kwenye Kanisa la Mtakatifu 
JosephMfanyakazi  eneo La olasiti Nje kidogo ya Jiji la Arusha.
 Akizungumza wakati akitoa 
Mablanketi kwa niaba ya wizara ya utalii kupitia shirika la hifadhi la 
taifa (TANAPA)Naibu waziri wa Maliasili na utalii Lazaro Nyalandu 
alisema kuwa wizara yake kupitia Tanapa wametoa vifaa hivyo ili kusaidia
 hospitali hiyo yenye huba wa madawa na vifaa mbali mbali ikiwemo 
upungufu wa vitanda,madawa na mablanketi ambayo sehemu ya madawa 
itakabidhiwa jioni na Mh.waziri mkuu kwa niaba ya serekali.
 “Kwanza tunatoa pole kwa majeruhi
 wote waliopatwa na tukio hilo na tunawatakia wapone haraka pili msaada 
huu tunautoa kwa ajili ya kupunguza upungufu uliotokea kwenye hospitali 
yetu ntakaa na wenzangu wadau wa utalii tuangalie nini cha kufanya” 
alisema nyalandu.
 Alisema kuwa jumla ya tsh.16.2 
milion zitatumika kununulia madawa ambayo ya takabidhiwa jioni na waziri
 mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Peter Pinda.
 Wakati huo huo kijana wa miaka 16
 mkazi wa Olasiti James Gerald amefariki dunia usiku wa kuamkia Leo 
ikiwa ni mtu wa pili kufariki katika tukio la mlipuko wa bomu uliotokea 
kwenye kanisa la Joseph Mfanyakazi kwenye kata ya Olasit jijini Arusha,
 Akithibitisha kutokea kwa mauti 
hayo Kaimu mganga mkuu wa Hospitali ya Mount Meru dkt.Mariam Murtazah 
alisema kuwa hospitali hiyo ilibidi kuongeza dawa kutokana na wingi wa 
watu na kuwa msaada waliupata umekuja wakati muafaka kwani hospitali 
hiyo inakabiliwa na upungufu wa vifaa yakiwemo madawa.
 Aidha Askofu mkuu wa JImbo kuu la
 katoliki Arusha Josephat Lebulu Akiongozana na Balozi wa Vatikan hapa 
nchini Fransisco Padilla waliwatembelea majeruhi wa mlipuko wa mabomu 
majra ya saa 11;39 na kuwafariji majeruhi hao kwa kuwawekea mkono wa 
Baraka kwenye mapaji ya uso.
 Akizungumza na waandishi wa 
habari baada ya kutoka kuwatembelea majeruhi hao alisema wamepata salamu
 mbali mbali kutoka mataifa mbali mbali wakiwatakia majeruhi hao wapone 
haraka na rambi rambi kwa wafiwa huku akitoa tamko la kanisa kuwa ni 
mafundisho ya bwana yesu kuwa tuushinde ubaya.
 Lebulu aliwataka wakirsto hapa 
watanzania kuweka ulinzi wao moyoni badala ya kutegemea polisi kwani 
majaribu ya shetani ni mengi kama unavyoona shetani anatumia watu kupiga
 mabomu hadi kwenye nyumba za ibada,hata ukiweka ulinzi kwenye nyumba za
 ibada bado shetani ataendelea kuwatumia wafuasi wake.
 “Tuweke ulinzi rohoni mwetu 
kwanza kabla ya kuuweka mbele ulinzi wa Askari wetu hakika kama 
hatutatumika na shetani basi matukio kama haya yatakuwa historia”alisema
 Lebulu mbele ya balozi Padilla


0 comments:
Post a Comment