Na Baraka Mpenja 
Mabingwa
 wapya wa ligi kuu Tanzania bara klabu ya Yanga ya Dar es salaam “Wazee 
wa Uturuki” wanaendelea kuimarisha mawindo yao juu ya watani zao wa jadi
 waliovuliwa taji msimu huu, wekundu wa Msimbazi Simba “Taifa kubwa” 
utakaopigwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam mei 18 mwaka huu.
Afisa habari wa klabu ya Yanga, Baraka Kizuguto ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa
 wachezaji wanaisubiri kwa hamu mechi hiyo ambayo ni maalumu kwao 
kunogesha ubingwa wao walioutwaa msimu huu kwani wasiposhinda mechi hiyo
 taji lao litaingia shubiri.
“Tunaendelea
 vizuri na mazoezi, wachezaji wote wapo salama na tunahitaji ushindi 
katika mchezo wetu wa mwisho ambao tutapambana na watani wa jadi Simba 
ambao mechi za mwisho wanakuja vizuri, lakini tunaimarisha mawindo 
yetu”.  Alisema Kizuguto.
Kizuto alisisitiza kuwa Yanga wamejipanga sana msimu huu na kuwazuia katika mchezo wowote ule ni kazi ngumu sana.
Afsia
 habari huyo alisema wachezaji wa Yanga “Watoto wa Jangwani na Twiga” 
wamekuwa wakiambiwa kuwa raha ya ubingwa ni kumpiga mtani wako, hivyo 
maandalizi ni mazuri na lazima washinde mechi hiyo ya mwisho.
“Kila
 mchezaji wetu anajua wajibu wake, Simba ni timu nzuri na vijana wao 
wanacheza kwa uzuri, lakini sisi tunajipanga barabara”. Alisema 
Kizuguto.
Pia 
alisema Yanga inayoongozwa na wachezaji nyota kama Haruna Hakizimana 
Fadhil Niyonzima, Khamis Kiiza, Frank Domayo, Simon Msuva na wengine 
wengi itacheza soka safi na la kuvutia mbele ya maelfu ya mashabiki wa 
klabu hizo.
Wakati
 Yanga wakijiwinda na mechi hiyo, Simba waliopo nafasi ya tatu 
wakijikusanyia pointi 42 kibondoni baada ya kushinda mchezo wa jana 
dhidi ya Ruvu Shooting mabao 3-1 uwanja wa taifa, wao wamebakiza mechi 
mbili ambapo kesho kutwa jumatano watashuka dimbani kuvaana na maafande 
wa Mgambo JKT kutoka jijini Tanga.
Kwa 
mujibu wa kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kiwhelu “Julio Alberto”, 
alisema kwa sasa timu inaandaliwa kwa ajili ya mchezo wa kesho kutwa na 
baada ya hapo watahamishia akili zao katika mchezo wa watani wa jadi mei
 18 mwaka huu.
“Kila
 mtu anaona maendeleo ya timu, vijana wanaimarika kila mechi, nadhani 
mechi  dhidi ya Yanga tutawafunga na kubakisha heshima yetu pale pale”. 
Alisema Julio.


0 comments:
Post a Comment