Na Baraka Mpenja 
Wajelajela
 Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya “Jiji la kijani” wanatarajia 
kuanza safari yao hapo kesho kuja jijini Dar es salaam kwa ajili ya 
mchezo wao wa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Maafande wa jeshi la 
kujenga Taifa JKT Ruvu dimba la Chamazi Mbande nje kidogo ya jiji la Dar
 es salaam siku ya mei mosi mwaka huu.
Katibu mkuu wa Tanzania Prisons Sadick Jumbe  ameiambia MICHEZO BOMBA!  kuwa
  kikosi chao mpaka sasa kipo salama na kimejiandaa kwa muda mrefu 
kuwakabili JKT Ruvu ambao kwa sasa wana morali kubwa ya kupambana 
kubakia ligi kuu msimu kutokana na kupata matokeo ya ushindi mchezo 
uliopita dhidi ya vibonde wa Ligi hiyo Africa Lyon ya jijini Dar es 
salaam.
“Kocha
 wetu Jumanne Chale amefanya mazoezi ya nguvu kujiandaa na mchezo huo, 
tuko nafasi ya tisa kati ya timu 14 tukiwa na pointi 26 sawa na 
wapinzani wetu, lakini malengo yetu ni kushinda mchezo huo ili kujiweka 
nafasi nzuri katika msimamo wa ligi”. Alisema Jumbe.
Katibu
 huyo aliongeza kuwa kwa sasa timu ina morali kubwa kutokana na wadau wa
 jijini Mbeya kujitokeza kwa wingi kuwapa sapoti wakiongozwa na kamanda 
wa polisi mkoani humo, Diwani Athman Msuya ambaye anaongoza kamati ya 
saidia Prisons ishinde.
“Tunakuja
 Dar es salaam tukiwa kamili gado, lazima niwaambie mashabiki kwamba 
kikosi chetu kwa sasa kipo imara na wachezaji wote wapo katika hali 
nzuri, tutapambana sana na maafande wenzetu ili kupata matokeo ya 
ushindi”.
Wakata
 huo huo maafande wa JKT Ruvu wakiwa chini ya mwalimu Keny Mwaisabula 
”mzazi” na msaidizi wake Greyson Haule wanaendelea na mazoezi kujiandaa 
na matanange huo wa kukata na mundu.
Akizungumza
 leo hii, Haule ambaye ni kocha msaidizi wa klabu hiyo alisema wana 
uhakika wa kupata matokeo ya ushindi mbele ya Prisons kwani kikosi kipo 
sawa ka mechi zote zilizosalia.
“Tuliwafunga
 Lyon na kupata pointi tatu na kufikisha 26 sawa na Prisons, hakika 
tunasakama kwa nguvu zote pointi nyingine tatu mbele ya wanajeshi 
wenzetu, lazima tuwaadabishe siku hiyo”. Alisema Haule.
Timu 
hizo mbili zote zina pointi 26 katika nafasi ya tisa na kumi, lakini 
Prisons wapo juu ya Ruvu kufuatia wastani mzuri wa mabao ya kufunga na 
kufungwa.


0 comments:
Post a Comment