
Kocha huyo alipohojiwa jijini Dar es Salaam baada ya mazoezi ya timu hiyo Uwanja wa Leader Club alisema kuwa kosa la Sunzu ni moja ambalo amekuwa hakubaliani nalo la kuondoka mazoezini bila taarifa. "Sina tatizo na Sunzu. Nafikiri wakati nawapa mikono, alikuwa mbali. Kwa hiyo sikuona kama ni lazima kumfuata." Mbali na hilo alisema; "Anatakiwa akubali majukumu ya timu. Lakini bado mahitaji athibitishe maandishi kwa uongozi na baada ya hapo, uongozi na mimi tutakaa kujadili suala lake kuona tutakubaliana vipi."
Alieleza kuwa kosa la kwanza Sunzu alifanya walipokuwa kambini Zanzibar mashindano ya Mapinduzi aliondoka bila taarifa na la pili ni hili la kususia mazoezi Uwanja wa Etihad Mwananyamala ambao Simba ilikuwa ikiutumia kwa mazoezi yake.
0 comments:
Post a Comment