Thursday, April 18, 2013

thm_tUHBFgSWlM
MBWANA MAKATA

tff_LOGO1Na Baraka Mpenja
Kufuatia malalamiko mengi juu ya waamuzi wakati huu wa ngwe ya lala salama ya ligi kuu soka Tanzania bara, shirikisho la kandanda Tanzania limeshauriwa kufanyia uchunguzi suala hilo ili kujua hali halisi ya jambo hilo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na FULLSHANGWE, aliyekuwa kocha wa maafande wa JKT Oljoro siku za hivi karibuni Mbwana Makata, alisema malalamiko siku zote yanaweza kuwa ya kweli au uzushi tu, lakini TFF wanatakiwa kufanyia kazi kwa uangalifu mkubwa.
“TFF kupitia kamati zake wanatakiwa kufumbua macho juu ya jambo hili, ligi inafikia ukingoni na kuna lawama nyingi kwa waamuzi, kinachoatakiwa kufanyika ni kukaa chini na kuunda kamati za kuchunguza suala hilo ili haki itendeke”. Alisema Makata.
Makata aliongeza kuwa ligi inafikia ukingoni, ushindani ni mkubwa sana hususani kwa timu zinazopigana kufa na kupona kukwepa mkasi wa kushuka daraja msimu huu hivyo kuna haja ya kuiangalia kwa jicho la darubini na kubaini udanganyifu uliopo.
Kocha huyo mwenye historia ya kucheza soka na kufundisha timu nyingi alisisitiza kuwa kwa sasa kuna kamati zinazoundwa kisiasa kwa madai kuwa zinasaidia timu zao zisishuke daraja, lakini kamati hizi zinatia mashaka kutokana na kuundwa wakati ligi inafikia ukiongoni.
“Mimi nashangaa sana, nasikia viongozi wa serikali wanajiingiza kuunda kamati za kusaidia timu isishuke daraja, kama kweli wana nia ya kuisaidia timu kwanini wasingejitokeze mapema?, timu ina hali mbaya ndio wanakuja kuisaidia, hapa ndipo wasiwasi unaibuka”. Alisema Makata.
Makata aliwata viongozi wanaojitokeza kusaidia timu wakati mambo yamekuwa magumu kuacha tabia hii na kama lengo lao ni hilo basi wajitokeze mwanzoni mwa msimu wakati timu inajiandaa kuanza michuano ya ligi na si ngwe ya lala kwa buriani .
Akizungumzia hali halisi ya ligi yetu, Makata alisema ligi ina ushindani mkubwa sana lakini kuna ulazima wa TFF na wadhamini wa ligi kubadili mfumo wa utoaji wa zawadi.
“Wajitahidi kutoa zawadi kwa timu zote zinazosalia ligi kuu, hii itapelekea timu kushindana kupata zawadi za nafasi nyingine mbali na nafasi ya kwanza, ikiwa hivi ligi itakuwa ya kuvutia sana”. Alishauri Makata.
Pia Makata imezishauri timu kushindani hadi dakika ya mwisho hata kama zina uhakika wa kubakia  ligi kuu.
Makata ni mchezaji wa zamani wa timu ya Waziri Mkuu Dodoma miaka ya sabini na themanini, Tukuyu stars “Banyambala” miaka ya themanini na Dar Young Africans miaka ya themanini na tisini.
Baada ya hapo alianza ukocha mwaka 1999 na klabu ya Mji Mpwapwa ya Dodoma aliyoipandisha daraja, Twiga ya Kinondoni ambayo baadaye ilinunuliwa na Pan Africans, na baadaye alijiunga na vijana wa mitaa ya kishamapanda ya mwanza Toto Africans na siku za hivi karibuni alikuwa na maafande wa JKT Oljoro lakini sasa amebwaga manyanga kuwafua wanajeshi hao.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video