UWANJANI
 White Hart Lane, Tottenham Hospur leo wameitandika Manchester City Bao 
3-1 na kujipa matumaini ya kuwemo kwenye 4 Bora ili kucheza ligi ya 
mabingwa Ulaya Msimu ujao na pia kuwakata maini Man City matumaini yao 
finyu ya kutetea Taji lao la Ubingwa ambalo kesho Usiku linaweza 
kuchukuliwa na Mahasimu wao Manchester United ikiwa wataifunga Aston 
Villa Uwanjani Old Trafford.
City 
walitangulia kufunga Bao mapema kupitia Samir Nasri katika Dakika ya 5 
lakini Bao 3 ndani ya Dakika 6 na Sekunde 20 kuanzia Dakika ya 75 
zilizofungwa na Clint Dempsey, Jermain Defoe na Gareth Bale 
 ziliwasambaratisha Man City.
Tottenham
 sasa wamefungana Pointi na Chelsea iliyo nafasi ya 4 lakini wanaweza 
kuishusha Arsenal iliyo nafasi ya 3 ikiwa watashinda Mechi yao moja 
waliyonayo mkononi.
VIKOSI:
Tottenham: Lloris, Walker, Dawson, Vertonghen, Assou-Ekotto, Sigurdsson, Dembele, Parker, Bale, Dempsey, Adebayor
Akiba: Friedel, Huddlestone, Naughton, Defoe, Holtby, Livermore, Caulker.
Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Nastasic, Clichy, Toure, Barry, Milner, Tevez, Nasri, Dzeko
Akiba: Pantilimon, Lescott, Sinclair, Kolarov, Javi Garcia, Aguero, Kolo Toure.
Refa: Lee Mason


0 comments:
Post a Comment