Watanzania wametakiwa kuacha mawazo potofu juu ya
mgawanyo wa rasilimali zilipo nchini kwa sababu zinatumika kwa ajili ya
wananchi wote pasipo upendeleo.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa nishati na madini
Profesa Sospeter Mhongo wakati akitoa ufafanuzi kufuatia maandamano ya wananchi
mkoani Mtwara kudai gesi inayochimbwa mkoani humo kutowanufaisha.
![]() |
Profesa Sospeter Mhongo |
Profesa Mhongo amesema maandamano kama hayo
yanaweza kuligawa taifa kwa sababu kila mkoa unatoa rasilimali zake ambazo
zinatumika na wananchi wa mikoa yote
bila kujali ukanda wa mikoa husika.
Waziri huyo amesema endapo wananchi wa kila mkoa wataandamana ni hatari kwa
amani, utulivu na ustawi wa taifa.
Amewataka wanasiasa kuangalia maslahi ya kiuchumi
kwa Taifa badala ya kuwapotosha wananchi na kusababisha mivutano isiyokuwa ya lazima katika jamii.
Profesa Mhongo amesema serikali inaamini ujenzi wa
bomba la gesi asilia kutoka Mnazi Bay mpaka jijini Dar es Salaam utalinufaisha
zaidi taifa kwa kutumiwa katika viwanda,taasisi na matumizi ya kawaida ya majumbani.
0 comments:
Post a Comment