Tuesday, January 22, 2013


Shujaa wa Azam leo, Mwaipopo

AZAM FC ya Dar es Salaam imemaliza vema ziara yake ya wiki moja nchini Kenya, baada ya kuifunga timu ya Benki ya Biashara Kenya, KCB bao 1-0 kwenye Uwanja wa City, Nairobi jioni hii.
Bao pekee la ushindi la Azam jioni hii limefungwa na kiungo Ibrahim Mwaipopo kwa shuti la mpira wa adhabu katika dakika ya pili ya muda wa nyongeza, baada ya kutimu kwa dakika 45 za kawaida za kipindi cha kwanza.
Hata hivyo, Azam ingeweza kuondoka na ushindi mnene zaidi leo, kama si kiungo wake mwingine Abdulhalim Humud ‘Gaucho’ kukosa penalti dakika ya 83 baada ya shuti lake la kudakwa na kipa wa KCB.
Huo unakuwa ushindi wa pili katika mechi zake tatu za kujipima nguvu nchini humo, kwani awali bao pekee la Gaudence Exavery Mwaikimba kwa penalti dakika ya 58 juzi liliipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Sofapaka ya Kenya kwenye Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Katika mchezo wake wa kwanza, mabingwa hao wa Kombe la Mapinduzi walifungwa mabao 2-1 na AFC Leopard kwenye Uwanja huo huo wa Nyayo.
Pamoja na kufungwa na Leopard, Azam watajilaumu wenyewe, kwani walipoteza penalti mbili kupitia kwa Joackins Atudo na Khamis Mcha ‘Vialli’.
Mabao ya Leopard katika mchezo huo, yalifungwa na Paul Were na Mike Barasa, wakati la Azam lilifungwa na Sammih Hajji Nuhu kwa penalti.
Katika mchezo wa leo, kikosi cha Azam FC kilikuwa; Mwadini Ally, Malika Ndeule, Samir Hajji Nuhu, David Mwantika/Omar Mtaki, Joackins Atudo, Kipre Balou/Abdulhalim Humud, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo/Humphrey Mieno, Abdi Kassim, Brian Umony/Uhuru Suleiman na Khamis Mcha/Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Azam kesho watapanda basi lao kuvuka boda la Namanga kurejea nyumbani Dar es Salaam, tayari kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.

Imehamishika kutoka kwa Bin Zubeiry leo

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video