
Maafande
wa Polisi Morogoro chini ya kocha mkuu wake John Simkoko wanaingia kambini leo
usiku mjini Morogoro kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara
unaotaraji kuanza kushika kasi januari 26 mwakani.
Afisa
habari wa klabu hiyo Clemence Banzo amesema wameingia kambini kwa lengo moja la
kufanya maandalizi ya kutosha ili kujinusuru kuingia mstari mwekundu wa
lkushuka daraja.
Banzo
amesema ili kuhakikisha wanaongeza nguvu, wamesajili wachezaji sita wakiwemo
Chacha Marwa aliyekuwa mchezaji huru, Salum Machaku kutoka Mtibwa sugar, Victor
Bundala kutoka Mtibwa na wengine wengi ambao atawataja hapa.
Pia
amese wachezaji hao wamesajiliwa kutoka na ripoti ya kocha wao John Simkoko
aliyetaka kukiongezea nguvu kikosi chake.
0 comments:
Post a Comment