Azam
 ya Dar es Salaam na Coastal Union ya Tanga ndizo zitakazoumana kwenye 
fainali ya michuano ya Kombe la Uhai 2012 itakayochezwa kesho jioni 
(Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es 
Salaam.
Timu
 hizo zimepata fursa hiyo baada ya kushinda mechi zao za nusu fainali ya
 michuano hiyo inayoshirikisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 
20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom. Michuano hiyo inayodhaminiwa na 
kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai.
Azam
 ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata tiketi ya fainali baada ya kuitoa 
Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa mikwaju ya penalti 3-2. Matokeo ya dakika 
90 yalikuwa bao 1-1. Nayo Coastal Union iliivua ubingwa Simba kwa 
kuifunga mabao 2-1.
Mechi
 ya fainali itaanza saa 10 kamili jioni, na itatanguliwa na ile ya 
kutafuta mshindi wa tatu kati ya Mtibwa Sugar na Simba ambayo itachezwa 
saa 2 kamili asubuhi kwenye uwanja huo huo.
Mbali
 ya kombe, bingwa wa michuano hiyo atapata sh. milioni 1.5, makamu 
bingwa sh. milioni 1 wakati mshindi wa tatu atajinyakulia sh. 500,000. 
Timu iliyoonesha zaidi mchezo wa kiungwana (fair play) itapata sh. 
400,000, mchezaji bora wa mashindano sh. 350,000, mfungaji bora sh. 
300,000 na kipa bora sh. 300,000.
Naye kocha bora katika mashindano hayo atazawadiwa sh. 300,000 kama itakavyokuwa kwa refa bora.

0 comments:
Post a Comment