| Hassan Kessy | 
Msuluhishi wa kisheria wa sakata la madai ya Simba dhidi ya Young 
Africans hali kadhalika Mchezaji Hassan Hamisi Ramadhani maarufu kama 
Hassan Kessy, Wakili Msomi, Mzee Said El-Maamry anatarajiwa kukutana na 
pande zinazopingana Alhamisi Novemba 3, mwaka huu ili kufikia mwafaka wa
 mwadai hayo.
Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji iliagiza pande za 
Simba na Young Africans kumaliza suala hilo mapema mwezi uliopita, 
lakini kwa sababu zilizo nje ya TFF na Kamati yake walishindwa kufanya 
hivyo kupewa barua ya wito kuitwa kikaoni Oktoba 29, mwaka huu.
Hata hivyo, msuluhishi huyo alishindwa kuendelea na kikao hicho baada
 ya taarifa kutoka Young Africans kusema kwamba mmoja wa Wawakilishi 
wake, Wakili Msomi Alex Mgongolwa kuwa safarini Iringa alikokwenda kwa 
sababu ya matatizo ya kifamilia. Ilielezwa kuwa Mgongolwa ambaye ni 
Mwanasheria wa Young Africans, alifiwa hivyo kuomba kupangiwa siku 
nyingine.
Kutokana na hali hiyo, E-Maamry amepanga sasa kukutana nna viongozi 
na/ au Wawakilishi wa pande zote mbili Alhamisi saa 11.00 jioni kwenye 
ofisi za TFF ili kuketi chini ya kuangalia namna ya kumaliza madai ya 
Simba iliyowasilisha mashauri mawili ambako moja ni dhidi ya Young 
Africans ilihali jingine ni dhidi ya mchezaji Hassan Kessy.
Mzee El-Maamry amesema: “Ili kutenda haki, lazima tutoe nafasi kwa 
pande zote kusikiliszwa. Ni vema Mwanasheria wa Young Africans 
akasubiriwa.”
Kamati ya TFF inasuburi makubaliano hayo, na ikitokea imeshindikana, 
suala hilo litarudi kwenye Kamati hiyo kwa ajili ya uamuzi wa mwisho kwa
 mujibu wa taratibu, kanuni na sheria zinazoongoza mpira wa miguu.

0 comments:
Post a Comment