Wednesday, November 30, 2016

Club Libertad wamejitolea wachezaji wao wote wa kikosi cha kwanza kuwapa timu ya Chapecoense kufuatia ajali mbaya ya ndege waliyopata timu hiyo ambapo watu 76 kati ya 81 wamefariki dunia.

Wakiwa njiani kusafiri kuelekea mchezo mkali na wa kihistoria kwao, klabu ya Chapecoense ilikuwa icheze mchezo wa fainali ya Copa Sudamericana dhidi ya Atletico Nacional lakini ajali iliyowakumba njiani ilihitimisha uhai wao.

Klabu hiyo ya Paraguay 'Club Libertad' walifungwa na kutupwa nje ya mashindano na Chapecoense kwa mikwaju ya penati katika hatua ya roo fainali ya michuano hiyo.

Taarifa kutoka klabu hiyo inasomeka hivi;

"Uongozi na timu nzima ya Club Libertad unaungana na wahanga kutoa salamu za rambirambi, kutokana na maafa yaliyowakuta ndugu zetu wa klabu ya ASOCIACION CHAPECOENSE DE FUTBOL na kuamua kutoa wachezaji wote wa kikosi cha kwanza kwa Chapecoense endapo kutakuwa na tukio lolote la kimichezo kwenye nchi yao. Tutoa pole kwa pigo la kuondokewa na wachezaji muhimu si tu kwa klabu bali kwa taifa pia."

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video