Mshambuliaji mpya wa Arsenal aliyesajili kutoka Deportivo La Coruna Lucas Perez leo amefungua ukurasa wa ambao kwa kufunga magoli mawili kwenye ushindai wa 4-0 kwa Arsenal kwenye mchezo wa Kombe la EFL dhidi ya Nottingham Forest inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza na kufanikiwa kufuzu raundi ya nne
Granit Xhaka alikuwa wa kwanza kufunga goli baada ya kupiga shuti kali kutoka umbali wa mita 30 na kuipa Arsenal goli la kuongoza.
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Nicklas Bendtner almanusura afunge bao lakini shuti lake lilitoka nje.
Baadaye Lucas Perez aliifungia Arsenal bao la pili kwa penati baada ya Chuba Akpom kufanyiwa madhambi kwenye eneo la hatari.
Lucas kwa mara nyingine tena alifunga bao tatu na la pili kwa upande wake kabla ya Alex Oxlade-Chamberlain kuhitimisha karamu ya ushindi kwa kufunga bao la nne mnamo dakika ya 90.
0 comments:
Post a Comment