Everton imeshinda 3-0 dhidi ya Southampton katika mechi ya mapema ya ligi kuu soka nchini England.
Romelu Lukaku aliifungia Everton magoli mawili katika dakika ya 22 na 45, huku bao la tatu likifungwa na Ross Barkley dakika ya 84.
Moja ya tukio la kuvutia katika mechi hiyo ni kitendo cha shabiki mmoja wa Southamoton kubabuliwa na mpira uliotokana na shuti la Lukaku akiwa amekaa jukwaani kabla ya mechi kuanza.
Baada ya tukio hilo, Lukaku alionesha upendo na kupanda jukwaani kwa lengo la kumpa pole shabiki huyo.
Alimkumbatia kwa muda mrefu mwanamke huyo kabla ya kusalimiana na mwanaume aliyekaa karibu na mwanamama huyo.
Pia alionekana akimpatia jezi shabiki wa Everton na kisha akashuka kuendelea na maandalizi ya mechi hiyo.

Romelu Lukaku akienda jukwaani kumpa pole shabiki baada ya shuti lake kumbabua

Lukaku akirudi uwanjani kuendelea na mazoezi

0 comments:
Post a Comment