Thursday, June 18, 2015

Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 15 (U-15) kitaingia kambini siku ya jumatatu tarehe 22/06/2015 ili kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya kombaini ya mkoa wa Mbeya, mchezo utakaofanyika mjini Mbeya jumatatu ya tarehe 28/06/2015.
Kikosi hiki kinaandaliwa kwa ajili ya kujiandaa na na michuano ya mtoano kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitakazofanyia nchini Madagascar mwaka 2017. Hatua ya mtoano wa awali itaanza mwakani 2016 mwezi Juni.
Timu itakua chini ya kocha Bakari Shime kwa muda akisaidiwa na Peter Manyika. Kocha aliyekua ameteuliwa awali kufundisha timu hiyo Adolf Rishard ameomba udhuru baada ya kupata fursa ya kwenda masomoni.
Wachezaji watakaoingia kambini na mikoa wanayotokea kwenye mabano ni Mwijuma Yahya (Tanga), David Mpakazi, Shilole Anthony (Geita),  Kibwana Shomari , Ibrahim Koba, (Morogoro), Faraji John, Kelvin Deogratius, Davison Meddy , Maulid Lembe (Dodoma), Ally Msengi (Mwanza).
Wengine ni Timoth Timothy, Juma Juma, Pius Raphael, Mohamed Ally (Dodoma), Athumani Rajabu, Juma Zubeir, Jonathan Rafael (Kigoma), Robert Philip, Jaffari Juma (Arusha), Michael Kanuti, Alex Peter, Rashid Kilongola (Kinondoni), Morris Michael (Ilala), Karim Mfaume (Lindi), Assad Juma (Unguja Magharibi), Francis Mrope, Kelvin Pius (Mara)

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video