Tuesday, May 12, 2015


Hii ni njia inayotumika kutambua mpira uliovuka mstari wa goli katikati ya nguzo mbili zilizosimama na ile nguzo inayounganisha nguzo mbili zilizosimama (mtambaa wa panya) pamoja na mstari uliochorwa chini ya mtambaa wa panya pia vifaa vya umeme/ kielekroniki (electronic devives) hutumika katika kumsaidia refa kuzawadia goli au la.

Lengo la teknolojia ya goli si kuondoa  kazi za waamuzi bali kuwasaidia katika kufanya maamuzi. Teknolojia ya goli ni lazima ioneshe wazi kama mpira wote umevuka mstari na hii taarifa itatumika kumsaidia refa katika kufanya maamuzi yake ya mwisho. Baada ya malumbano na mijadala mbalimbali kuibuka katika ligi kuu ya Uingereza, Kombe la Dunia – 2010, na Kombe la Mataifa ya Ulaya – 2012, FIFA (ambayo mwanzoni ilikuwa ikiipinga teknolojia hii) iliamua kupima teknolojia tisa lakini ni mbili tu zilizokubalika.

Tarehe 5 Julai 2012, Bodi ya Kimataifa ya Mpira wa Miguu (IFAB – International Football Association Board) iliruhusu matumizi ya teknolojia ya goli, na kubadilisha sheria za mchezo kuruhusu (lakini si kulazimisha) matumizi.

Ni mifumo (Systems) miwili tu ndio ilipitishwa kutumika, wa kwanza ukiwa ni Goli la Refa (GoalRef) na wa pili ukiwa ni wa Jicho la Mwewe (Hawk-Eye). Desemba 2012, FIFA ilitangaza kuitumia teknolojia ya goli katika mechi za mashindano kwa mara ya kwanza katika Kombe la Dunia – 2014. Kuanzia mwaka 2013, teknolojia hii ilianza kutumika katika ligi kuu ya soka nchini Marekani lakini timu za Canada zinazoshiriki ligi hiyo hazitumii teknolojia hii zinapocheza nyumbani kutoka na ukosefu wa fedha.

Teknolojia ya goli iliwekwa katika viwanja vyote 12 vilivyotumika katika Kombe la Dunia – 2014 nchini Brazili. Teknolojia hii sasa inatumika katika ligi maarufu zaidi kwa kandanda duniani, Ligi Kuu ya Uingereza.


Sheria

Tangu 2012, sheria hii imeruhusiwa kutumika kwenye mechi. Lakini pia si lazima kuitumia, gharama yake na upya wake katika jamii ya wanasoka inamaanisha inaweza kutumika katika mechi za mashindano makubwa tu.

Haya ni baadhi ya maneno yanayoweza kupatikana katika sheria za mchezo yakihusu teknolojia hii:

·         Sheria namba 1 (Uwanja wa mchezo): inaruhusiwa kufanya maboresho katika fremu ya goli.


·         Sheria namba 2 (Mpira): inaruhusiwa kutumia mpira ulio na teknolojia hiyo ndani yake.


·         Sheria namba 5 (Refa): inamtaka refa kupima kama teknolojia ya goli inafanya kazi kabla ya mechi na endapo atagundua mapungufu yeyote basi asiitumie.


·         Sheria namba 10 (Njia ya Ufungaji Goli) : Kuruhusu matumizi ya teknolojia ya goli ili kujua  kama goli limefungwa au la. Inasema, “Matumizi ya teknolojia ya goli lazima yaoneshwe kwenye sheria za mashindano husika”



Ukosoaji

Mawakili wa teknolojia ya goli wanaendelea kusema kuwa itapunguza makosa ya refa kwa sehemu wakati wa mchezo lakini bado kuna ukosoaji wa teknolojia hii umeendelea kuwepo. Ukosoaji mwingi umetokea ndani ya FIFA wenyewe pamoja na Rais wa FIFA, Sepp Blatter. Pamoja na kuwepo ukosoaji katika teknolojia mbili zilizopitishwa, wakosoaji wanasema itaondoa ile hali ya kibinadamu ndani ya mchezo na pia  itapunguza  ladha ya majadiliano yanayotokana na makosa yaliyofanyika katika mchezo husika. Sepp Blatter amewahi kunukuliwa akisema, “Michezo mingine imekuwa ikibadilisha sheria zake ili kuendana na  teknolojia mpya..... Sisi hatufanyi hivyo na hii inafanya mpira wa miguu uvutie sana na kuwa maarufu zaidi”

Wakosoaji wengine wanasema itakuwa ni gharama sana kuiweka teknolojia hii katika kila daraja la mchezo hasahasa katika vyama vidogo vya mpira na maskini. Watu wenye sauti FIFA wameelezea kupendezwa zaidi na dhana ya ‘Ubora wa maamuzi’ kwa kuongeza idadi ya marefa na sio kuitumia teknolojia hiyo.

Blatter yeye alikuwa akiipinga teknolojia hii hadi pale  goli la Frank Lampard wa Uingereza lilipokataliwa katika Kombe la Dunia – 2010 ambapo mpira ulionekana wazi kuvuka mstari wa goli.

Utambulisho wa  marefa watano yaani marefa wengine wawili kusimama nyuma ya goli kila goli moja refa mmoja, ilikuwa ni sehemu ya kusaidia matukio kama haya.




Gharama

Mwanzoni wa mwaka 2014, timu nyingi zinazoshiriki ligi kuu ya soka ya Ujerumani – Bundesliga walipiga kura ya hapana kukataa teknolojia hii ya goli kutokana na sababu za kifedha. Kila klabu moja ingetakiwa kutoa € 250,000 (zaidi ya milioni mia tano, shilingi za Tanzania) kwa ajili ya kuweka kadi ndani ya mpira hadi € 500,000 (zaidi ya bilioni moja, shilingi za Tanzania) kwa ajili ya teknolojia ya Jicho la Mwewe. Kocha wa klabu ya 1. FC Cologne, Jorg Schmadtke, alitoa majumuisho ya kura  kwa kusema, “Gharama ni kubwa sana na hii (teknolojia) haikubaliki”


Ilitazamiwa FIFA ingepata Paundi 300,000 kutokana na ligi kuu ya Uingereza kuamua kuitumia teknolojia hii. Kila klabu ilitoa Paundi 15,000 kwa ajili ya kuweka, kuipima na kupata nembo ya ubora wa FIFA kwa kamera za Jicho la Mwewe. Pia FIFA ilipata paundi zingine 15,000 kwa ajili ya Uwanja wa Wembley ambao hutumika katika mechi za nusu fainali na fainali za Kombe la FA pamoja na fainali ya Kombe la Ligi.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video