Wednesday, August 20, 2014

Third-party games: Rojo deal shows the buffet is still open for football's mystery guests
 HATIMAYE Manchester United imeingia katika hatihati kwa kumsajili beki wa Sporting Lisbon, Marcos Rojo, ingawa njia zilizotumika ni za uhamisho wa kisasa.

Kitendo cha United kuzungumza na mchezaji huyo wiki iliyopita kulisababisha mgongano baina ya Sporting na Kundi la Uwekezaji la Doyen Sports (walioshughulikia uhamisho wa Radamel Falcao kwenda Monaco na linamjumuisha mkurugenzi mkuu wa zamani wa Chelsea, Peter Kenyon na wakala mwenye nguvu kubwa, Jorge Mendes).


Doyen wanadai kuwa wanamiliki 75%  ya haki za kiuchumi za Rojo, na wameripotiwa kutaka kukata asilimia ya ada iliyolipwa na United, lakini suala hilo limekataliwa. United wamepitia rekodi na kusema suala hilo lina utata mkubwa.


Siku ya jumanne, Sporting walitangaza kupitia soka la hisa kuwa wamemuuza Rojo kwa dau la Euro milioni 20 (paundi milioni 16) na kusema kuwa watailipa Doyen fedha za uwekezaji wa awali ambazo ni milioni 3 (paundi milioni 2.4), lakini waligoma kutoa zaidi ya hapo.


Bado utata umeendelea kuwepo na hapo ndipo wamiliki wa kampuni ya ‘Third-party’ (TOP) inayohusika na masuala ya wuchezaji inaibua maswali ambayo hayana majibu kuhusu fedha, uchumi na usimamizi wa mauzo ya wachezaji..


Doyen kama wafadhili wa mpira wa miguu walieleza kuwa hawahusiki na kuwasimamia wachezaji au kusimamia uhamisho wao. “Hatumiliki wachezaji. Tunajihusisha benki ya Barclays au benki nyingine wakopeshaiji wa mikopo, lakini hatuwezi kudhibiti maisha au mshahara wa mchezaji. Sisi Kamwe hatufanyi chochote kinyume na matakwa yao”, alisema Mkurugenzi mtendaji, Nelio Friere alipoulizwa maswali juu ya TOP mwaka uliopita.


Third-party wanahusika na uwekezaji wa nje na kufikia makubaliano na klabu juu ya ada ya uhamisho na kuzitunza haki za kiuchumi za mchezaji anapouzwa.


Kuna makundi ya uwekezaji yaliyoanzishwa mahususi kwa masuala haya; moja wapo ni Doyen Sports ambao wamewekeza paundi milioni 80 kwa ajili ya kutunza vipaji vya wanamichezo duniani. (Kikosi walichotengeneza ni mchezaji wa Olympiakos, Alberto Botia na Manu del Moral wa Sevilla). Pia mchezaji wa kimataifa wa Hispania Alvaro Negredo, Falcao wa Monaco na mchezaji wa karibuni ambaye amesajiliwa na Manchester City, Eliaquim Mangala) nao walihusishwa na kampuni hii.


Kiukweli dili la kumchukua beki huyu wa zamani wa Porto, Mangala kwenda England halikuwa rahisi kwasababu halikuhusisha tu klabu bali Doyen nao walihusika. Kila mtu alitaka kupata chake katika ada ya uhamisho.


 Arrival: Marcos Rojo touched down in England on Tuesday ahead of a move to Manchester United
Akiwasili: Marcos Rojo alitua nchini England jana kukamilisha taratibu za usajili katika klabu ya Man United.

Uhamisho wa Falcao kutoka Porto kwenda Atletico Madrid mwaka 2011, Doyen Sports na Atletico waligawana ada ya uhamisho ambapo kila upande ulichukua 50%.


Hata alipouzwa katika klabu ya Monaco kwa Euro milioni 60, Atletico waligawana fedha iliyopatikana na wawekezaji hao.


Kwasasa kampuni ya TPO imepigwa marufuku nchini England, Ufaransa na Poland. Lakini katika maeneo mengine bado inaendelea kuwepo hususani Hispania, Ureno, Ulaya mashariki na Amerika kusini, hasa Brazil.


Kwa mujibu wa ripoti ya kampuni ya uhasibu ya KPMG, TOP kwa 27% na 36% wanamiliki wachezaji  katika soko la usajili nchini Ureno, na sasa namba imeongezeka na kufikia 40% kwa ligi za Ulaya mashariki.


Wakati kwa Hispania takwimu zinaonesha kuwa TOP wanahusika kwa 8%, na katika misimu ya karibuni, takwimu zimeongezeka kwa klabu za La Liga.


Nchini Brazil, 90% ya wachezaji wake wanaocheza ligi kuu, haki za kiuchumi zinamilikiwa na wawekezaji. Inafahamika kuwa suala hili limeleta faida na hasara.


UEFA na Rais wake Michel Platini hawawezi kulipuuza suala hili. Katika mkutano wa mwaka wa FIFA uliofanyika mwezi septemba mwaka jana alimuomba Rais wa FIFA, Sepp Blatter kutengeneza sheria ya kuwazuia TOP, akisema kuwa, “Tatizo la wachezaji kumilikiwa na makumpuni yenye misingi ya kodi  na mawakala wasiofahamika.


“Rahisi tu, baadhi ya wachezaji hawana uhuru katika masuala yao ya kisoka na wanauzwa kila mwaka ili watu wasiojulikana wavune mapato na kujipatia hela kutoka kwenye masuala ya mpira”.


Platini alitishia kwamba, kama FIFA na Blatter hawataweka sheria, UEFA italazimika kutengeneza sheria yake ili kukabiliana na vitendo hivi ambavyo anahisi ni ‘Hatari katika michezo’. Walipoulizwa juu ya madai ya Platini, Doyen Sport waligoma kuzungumza chochote.

Incoming:  Rojo is heading to Manchester United after they agreed a fee with Sporting Lisbon

Chama kinachosimamia wachezaji wa kimataifa cha FIFA, Fifpro Kiliweka wazi na kuunga mkono kauli ya Platini. Mkurugenzi wa mawasiliano Andrew Orsatti alisema kuwa chama hicho kinapingana na TOP kwa namba yoyote ile kwasababu kinakwenda kinyume na haki za wachezaji kama binadamu na wafanyakazi.


Inawezekana lengo la wawekezaji ni zuri, lakini ukweli ni kwamba uhusiano wa asiyenacho na mwenye nacho unazidi kuongezeka katika soka. Matajiri wakubwa wameingia katika soka kama vile Manchester City, Chelsea na Paris Saint-Germain ambao mamiliki wanamwanga fedha za kutosha katika soka la wachezaji na mishahara.

Miamba ya soka kama Manchester United na Barcelona imeongeza wigo wa mapato yake tangu mwaka 2010; Barca aliongeza kwa paundi milioni 48 kati ya 2012-13 na 2013-14, wakati Manchester United waliongeza paundi milioni 752 kwenye mkataba wa Adidas (unaoanza mwaka 2015).


Klabu kubwa zinaweza kujiendesha zenyewe, lakini fedha wanazopewa wanatakiwa kuzitumia katika misingi ya sheria ya matumizi ya fedha. Pesa inahitajika katika mpira na hapo ndipo TPO wanakuja.


Kitu cha kuvutia ni kwa klabu kama Atletico Madrid, Benfica na Porto ambazo hutumia TOP kwa kugawana hasara.


 Ripoti ya KPMG ilisema asilimia inayomilikiwa na Third-party haizidi asilimia 50, ni kati ya 10% na 40% ambayo inakubalika (lakini suala la Rojo limekuwa tofauti), kwa maana ya wamiliki wa nje ndio wana hisa kubwa zaidi katika maisha ya mchezaji huyo.


Javier Tebas, Rais wa chama cha soka la Hispania aliruhusu uwekezaji wa fedha katika soka kwa madai kuwa zitasaidia kuimarisha ushindani wa klabu za nchi hiyo.


Kutokana na maamuzi hayo, TPO ndio chaguo kwa klabu nyingi za nchi hiyo. Kwahiyo maombi ya Platini kupiga marufuku makampuni haya kama vile litashindikana, anaamini mwanasheria wa michezo wa FIFA, Alumni Luis Villas Boas Pires.


“Sidhani kama FIFA watapiga marufuku TOP,” aliuambia mtandao Goal.

“Kama Uefa wataamua kupiga marufuku TOP, maamuzi kama hayo yatachukuliwa dhidi ya sheria ya matumizi ya fedha ya Uefa”.


Lakini ukweli ni kwamba, hata kama TPO watapigwa marufuku au la, bado kuna utata mkubwa ambapo wawekezaji wanakuwa na nguvu zaidi juu ya wachezaji.


Kuna haja ya kuchambua vizuri wawekezaji hao hata kama hawatapigwa marufuku kama ilivyo kwa Ligi kuu Engalnd, lakini kamati ya utawala ya FIFA lazima ipewe nguvu ya kuweka sheria nzuri ya kudhibiti TPO ili kuokoa mpira wa miguu.


Mkurugenzi wa LFP, Tenas anaamini kuwa “sheria ya kuwasimamia ni TPO ni muhimu ikawekwa ili kulinda haki”.


Villas-Boas anaamini sheria ni muhimu kuanzishwa kwa lengo la kuzisaidia klabu juu ya suala hili, lakini kuwapiga marufuku moja kwa moja halitakuwa jambo jema.


Aliongeza: “Kupiga marufuku TPO hakutazuia wawekezaji kunua haki za kiuchumi za wachezaji- watatafuta ujanja juu ya katazo hilo.Kama Sheria nzuri, usimamizi mzuri juuya wamiliki wa haki za wachezaji itawekwa wazi, kutaifanya Uefa ipunguze wasiwasi wa athari hasi za TPO”.


 Kama ilivyo katika sheria ya matumizi ya fedha, kuna haja ya kuanzisha utaratibu mzuri. Mwanasheria wa michezo, Daniel Geey anasema njia pekee ya kupambana na TPO ni kutengeneza sheria inayowalazimu kuweka mambo yote hadharani.


“Kudhibiti TPO ni jambo gumu sana kutokana na utata uliopo juu ya mgongano wa kimasilahi,” aliueleza mtandao wa Goal.


Jambo la muhimu ni kwamba-TPO hawawezi kuzuiliwa, ukiangalia hali halisi ya klabu ya Valencia. Mjadala wa mgongano wa masilahi umeibuka ambapo mmiliki wake, Peter Lim alipewa mfuko wa uwekezaji ambao unahusisha wachezaji wawili waliosajiliwa majira ya kiangazi-Rodrigo Moreno na Andre Gomes.


Hali ya vikundi vya uwekezaji kujihusisha zaidi na masuala ya klabu, ni tishio katika michezo. Kwa maana hiyo kuna umuhimu wa kuanzishwa kwa sheria ya usimamizi wa TPO.


Hata hivyo, Fifpro na Orsatti ndio wenye mamlaka au uwezo kwa kushughulikia utata kama huu.


Wakati Uefa na FIFA wakifikiria cha kufanya baadaye, Doyen Sports mwezi Aprili walitangaza kutengeneza mkatati mpya wa pili ‘Doyen Sports II’-ambapo watawekeza zaidi katika michezo wakianza  na paundi milioni 160 kwa ajili ya kusajili wachezaji wapya wenye vipaji duniani.


Doyen wanakuja na mpango huu ambao unasemekana kupunguza uovu ili kukwepa kupigwa marufuku kimataifa. Hawataki suala la Rojo kutokea miaka ijayo.




0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video