Saturday, July 12, 2014


Thumbs up: Luis Suarez has completed a £75million move to Barcelona from Liverpool
Mmenisoma hapo?: Luis Suarez amekamilisha uhamisho wake wa paundi milioni 75 kutokea Liverpool kwenda Barcleona.
Back to work: Liverpool manager Brendan Rodgers pictured at the first pre-season training session on Monday
Karudi kazini: Kocha wa Liverpool  Brendan Rodgers alipigwa picha akiwa katika mazoezi yake ya kwanza ya maandilizi ya msimu siku ya jumatatu.

Imechapishwa Julai 12, 2014, saa 5:44 asubuhi

Brendan Rodgers amefunguka na kusema ataifanya Liverpool kuwa imara baada ya kumruhusu Luis Suarez kuondoka.
Kocha huyo wa Liverpool amemruhusu Suarez kwenda Barcelona baada ya wakatalunya hao kukubali kulipa dau la paundi milioni 75 na atatangazwa rasmi kama mchezaji wa Nou Camp wiki ijayo baada ya vipimo vya afya.
Msimu uliopita, Suarez alikuwa mfungaji bora wa ligi kuu England na mshindi wa tuzo ya PFA na Tuzo ya mchezaji bora wa mwaka inayotolewa na waandishi wa habari, hivyo kuondoka kwake imekuwa huzuni kwa mashabiki wa Liverpool.
Lakini Rodgers amewatuliza mashabiki wa majogoo wa jiji na kusema ataiboresha zaidi Liverpool, kwasababu klabu ni kubwa kuliko mtu mmoja.
And he's off: Rodgers (left) said that Liverpool did all they can to try and keep Suarez at Liverpool
Hayupo tena: Rodgers (kushoto) alisema Liverpool ilijaribu kwa kila namna kumbakisha Luis Suarez katika klabu ya Liverpool.
Banned: Luis Suarez has seen his appeal against his four-month ban for biting Giorgio Chiellini rejected
Amefungiwa: Luis Suarez amefungiwa miezi minne kwa kitendo cha kumng`ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini katika mechi ya fainali ya kombe la dunia.

Rodgers aliyemtetea Suarez baada ya kumng`ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic mwaka jana alisema: "Klabu imefanya kila jitihada ili kumbakisha Luis Suarez".
"Imekuwa ngumu kukubaliana baada ya majadiliano ya muda mrefu, na kwasasa tumeshakubaliana aende Hispania ili apate changamoto mpya"
Rodgers anakabiliana na changamoto ya kutafuta mbadala wa mchezaji aliyefunga mabao 31 msimu uliopita.
Mshambuliaji wa QPR, Loic Remy na wa Swansea, Wilfried Bony ndio wachezaji wanaowindwa zaidi.
Lakini Rodgers aliahidi: "Nina imani tutaimarisha timu zaidi na tutakuwa wakali zaidi msimu ujao. Kama kuna kitu cha kihistoria ambacho klabu hii inatufundisha, ni kwamba, Liverpool ni kubwa kuliko mtu binafsi. Natumaini mashabiki wetu wanaota na wanaamini kuwa tunakwenda mbele na tutaendelea kusonga zaidi, kwapamoja tutaleta mafanikio".

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video