Friday, March 14, 2014

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam


0712461976 au 0764302956


WANA Lambalamba Azam fc wamesema nia yao ya kutwaa ubingwa kwa mara ya kwanza msimu huu iko palepale japokuwa kuna ushindani mkubwa.

Akizungumzia maandalizi ya mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union katika uwanja wa Azam Complex , uliopo Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam, afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema kila kitu kinakwenda sawa.

“Msimu huu ligi imekuwa ngumu zaidi, kila timu imejipanga na ndio maana matokeo yasiyotegemewa yanapatikana. Sisi tunaendelea kupambana ili tubaki kileleni na kutwaa ubingwa wetu wa kwanza ligi kuu Tanzania bara”. Alisema Jafar.

“Coastal ni timu nzuri yenye ushindani mkubwa. Tunajua ugumu wa mchezo huo, lakini kocha wetu Joseph Marius Omog amewaandaa vijana wetu kutafuta ushindi”. Alisema Jafar.

Aidha Afisa habari huyo aliongeza kuwa hakuna timu dhaifu msimu huu na ndio maana timu inatoka kufungwa 6-0 halafu unakutana nayo inakufunga.

“Sisi ni timu pekee ambao hatujapoteza mchezo mpaka sasa. Malengo yetu ni kuktwaa ubingwa msimu huu. Tutapambana mpaka mwisho tuone matokeo yake”. Alisisitiza Jafar.

Naye Afisa habari wa Coastal Union, Hafidh Kido aliandika kwenye mtandao wa klabu hiyo kuwa wamejiandaa kukabiliana na kikosi cha Azam fc.

“Azam ni wazuri na hawajafungwa. Sisi pia ni wazuri, lakini hatujawa na matokeo mazuri sana. Tumejiandaa kupambana mwanzo mwisho katika mechi yetu hiyo muhimu ili kupata pointi tatu muhimu”. Alisema Kido.

Mpaka sasa Azam fc wapo kileleni wakiwa na pointi 40,  wakati Coastal Union wao wapo nafasi ya 7 wakiwa na pointi 26.

Mechi nyingine itachezwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kwa kuwakutanisha wenyeji Kagera Sugar dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya.

Nao Mabingwa watetezi Yanga wataumana na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video