NA Boniface Wambura, TFF
echi
 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Mbeya City iliyochezwa 
jana (Septemba 21 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam 
imeingiza sh. 123,971,000.
Watazamaji
 21,936 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 32 ya VPL 
msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2.
Viingilio
 katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 
20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 30,064,741.95 wakati Kodi ya
 Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 18,910,830.51.
Mgawo
 mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 15,287,156.92, 
tiketi sh. 3,145,790, gharama za mechi sh. 9,172,294.15, Kamati ya Ligi 
sh. 9,172,294.15, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 
4,586,147.08 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) 
sh. 3,567,003.28.


0 comments:
Post a Comment