Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
Manchester
 United leo hii wamepokea kipigo kikali zaidi katika dimba la the Etihad
 tangu mwaka 2004 baada ya kula 4-1 kutoka kwa wenyeji Manchester City.
Kwa 
matokeo ya leo, vijana wa David Moyes, Man United wameshuka mpaka nafasi
 ya nane katika msimamo wa BPL wakijikusanyia pointi 7 kibindoni, wakati
 Man City wenyewe wanabakia nafasi ya tatu wakiwa na mzigo wa pointi 10.
Nafasi
 ya kwanza kwa sasa inashikiliwa na washika bunduki wa kaskazini mwa 
London, klabu ya Arsenal chini ya kocha Mfaransa, Aserne Wenger wakiwa 
na pointi 12  sawa na Tottenham Hospurs wenye alama 12 sawa na Gunners 
katika nafasi ya pili, lakini wanatofautiana mabao ya kufunga na 
kufungwa.
Mshambuliaji
 hatari, Raia wa Arjentina, Sergio Aguero ametikisha nyavu mara mbili, 
huku nguli kutoka Ivory Coast, Yaya Toure na Mfaransa, Samir Nasri 
wakijipigia moja moja na kufanya kocha wa City Manuel Pellegrini aibuke 
kidedea katika mechi ya kwanza ya watani wa jadi wa jiji la Manchester 
nchini England, ` Manchester derby`.
Kikosi
 Manchester City: Hart 7, Zabaleta 7, Kompany 7, Nastasic 7, Kolarov 7, 
Jesus Navas 8 (Milner 71 6), Toure 8, Fernandinho 8, Nasri 9, Aguero 8 
(Javi Garcia 86), Negredo 8 (Dzeko 75).
Kikosi
 cha Manchester United: De Gea 5, Smalling 6, Ferdinand 6, Vidic 5, Evra
 6, Carrick 6, Fellaini 5, Valencia 5, Rooney 6, Young 5 (Cleverley 51 
6), Welbeck 6.
 
Mkali wa leo: Sergio Aguero amejipigia mawili katika ushindi wa City 
 
Bao la kwanza: Aguero akifunga bao lake la kwanza katika ushindi mnono wa 4-1
 
Mwafrika anayeujua mpira: Yaya Toure akipiga bao na kufanya ubao usomeke 2-0 kipindi cha kwanza
 
Mzee wa kazi: Yaya Toure akishangilia bao lake
 
Wazee
 kimenuka!: Wayne Rooney, Danny Welbeck na Michael Carrick wakiwa hawana
 hamu baada ya mvua kuendelea kuwanyeshea leo Etihad
 
Dogo tulia, hapa kazi tu!: Marouane Fellain  akionesha maujanja mbele ya Yaya Toure na nahodha Vincent Kompany
MECHI ZA LEO NA MATOKEO KWA UFUPI 
| 
 
Finished 
 | 
 
 Crystal Palace  
 | 
- | 
 
 Swansea  
 | 
(0-1) | ||||||
| 
 
Finished 
 | 
 
 Arsenal  
 | 
- | 
 
 Stoke  
 | 
(2-1) | ||||||
| 
 
Finished 
 | 
 
 Cardiff  
 | 
- | 
 
 Tottenham  
 | 
(0-0) | ||||||
| 
 
Finished 
 | 
 
 Manchester City  
 | 
- | 
 
 Manchester United  
 | 

0 comments:
Post a Comment