Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akiwapa 
nasaha wanamichezo wa wizara hiyo katika tafrija fupi ya kuwaaga 
wawakilishi wa wizara hiyo ambao watashiriki katika mashindano ya 
Shirikisho ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) 
yatakayofanyika mjini Dodoma Jumamosi. Tafrija ya kuwaaga wanamichezo 
hao ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Maafisa wa Polisi 
jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya 
Ndani ya Nchi.  
 
 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wa nne 
kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Wanamichezo wa Wizara ya
 Mambo ya Ndani ya Nchi baada ya kuwaaaga rasmi katika tafrija 
iliyofanyika Chuo cha Maafisa wa Polisi, jijini Dar es Salaam leo. 
Abdulwakil aliwataka wanamichezo hao wahakikishe wanashirikiana ipasavyo
 na hatimaye wanashinda michezo aina mbalimbali inayotarajiwa kuanza 
mjini Dodoma Jumamosi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani 
ya Nchi. 
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.


0 comments:
Post a Comment