Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mabingwa soka nchini England, klabu ya Manchester United leo hii imefanya mazoezi mazoezi ufukweni mwa bahari ambapo walisafiri kutoka bandari ya Sydney kwenda Ufukwe wa Bondi kwa njia ya boti.
Mazoezi hayo yamefanyika katika bichi ya Bondi kabla ya kukwea pipa kuelekea nchini Japan kuendelea na ziara ya ya kujianda na msimu mpya wa ligi kuu soka nchini England.
Vijana hao wa David moyes watakuwa na mechi tano za kirafiki nchini Japan na jumanne ya kesho kutwa watashuka dimbani kucheza na Yokohama F-Marinos mjini Yokohama.
Kufuatia ushindi wa mabao 5-1 walioupata jana dhidi ya A-League All Stars , kikosi hicho leo asubuhi kimefanya mazoezi fukwe za Bond.
Mambo ya ufukweni: Kikosi cha Manchester United kimefanya mazoezi katika Ufukwe wa Bondi
Maisha ya bichi hayo: Wachezaji wa United , kushoto kuelekea kulia, Anderson, Robin van Persie, Rafael da Silva na Tom Cleverley
Kocha wa United., David Moyes akipozi katika bandari ya Sydney kabla ya kupanda boti kuelekea ufukwe wa Bondi 

Mapumziko: Giggs, juu, na Wilfried Zaha chini wakipumzika ufukweni
Majembe: Phil Jones na Ben Amos wakiwasili ufukwe wa Bondi kwa ajili ya mazoezi
Kabla ya kupanda Boti: Lejendari Giggs akiwa katika bandari ya Sydney
0 comments:
Post a Comment