Na Joshua Mmali.
Oliver Mtukudzi alitoa burudani bure kwa wakazi wa New York katika eneo la kupumzika Free Park, maelfu ya wamarekani walifurika katika show yake. Hii inafundisha nini wasanii wa nyumbani Tanzania? Nafikiri kuna jambo kubwa sana la kujifunza toka kwa mkongwe huyu.
Oliver si mjinga kutoa burudani ya bure, wasanii wetu toka Tanzania inabidi waige mfano huu ili mziki wao uanze kuwaingia wamarekani na hata mataifa mengine ya nje. Nazungumzia msanii kujulikana na kukubalika katika kiwango cha kimataifa katika soko la mziki la dunia.

kuona mengi toka Swahili TV Mtaani Kunani tembelea www.swahilitv.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment