Na Baraka Mpenja 
Wekundu
 wa msimbazi Simba leo hii wametoa dozi nyingine  kwa maafande wa Mgambo
 Shooting kutoka mkoani Pwani baada ya kuwatungua bao 1-0 sifuri katika 
mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Mchezo
 huo uliotawaliwa na soka la ufundi umepigwa katika dimba la taifa 
jijini Dar es salaam na kushuhudiwa na mashabiki wengi wa Simba wenye 
matumaini makubwana kikosi chao kipya.
Mnyama
 sasa amefufua matumaini ya kucheza michuano ya Afrika mwakani, kufuatia
 ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Mgambo  leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar
 es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Katika
 mchezo huo, uliochezeshwa na refa Andrew Shamba, aliyesaidiwa na 
Abdallah Rashid na Abdallah Mkomwa wote kutoka Pwani, hadi mapumziko, 
Simba SC walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Bao 
hilo lilifungwa na kiungo hatari wa pembeni, Haroun Athumani Chanongo 
dakika ya nane, ambaye aliombea mpira katikati ya Uwanja na kuanza 
kuwapangua mabeki wa Mgambo kabla ya kumchambua kipa Godson Mmasa.
Ushindi
 huo, unaifanya Simba SC itimize pointi 45, sasa ikizidiwa tatu na Azam 
FC inayoshika nafasi ya pili, ambayo Jumapili itamenyana na Mgambo 
kwenye Uwanja wake wa Azam Complex, Chamazi.
 Katika
 mchezo wa leo, kocha Mfaransa Patrick Liewig aliwapumzisha wachezaji 
kadhaa tegemeo, Mrisho Ngassa, Shomary Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Felix 
Sunzu na Mussa Mudde kuelekea mchezo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, 
Yanga Mei 18.   
Kikosi
 cha Simba SC leo kilikuwa; Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’/Omary 
Salum, Haruna Shamte, Miraj Adam, Hassan Khatib, Jonas Mkude, Edward 
Christopher, William Lucian ‘Gallas’/Rashid Ismail, Amri Kiemba, 
Ramadhani Singano ‘Messi’/Salim Kinje na Haroun Chanongo.
JKT 
Mgambo; Godson Mmasa, Salum Mlima, Ramadhani Kambwili, Bashiru Chanacha,
 Bakari Mtama, Salum Kipanga, Chande Magoja/Mussa Gunda, Peter 
Mwalyanzi, Issa Kandulu, Fully Maganga na Nassor Gumbo


0 comments:
Post a Comment