Monday, April 8, 2013


PRISONS

Na Baraka Mpenja, Dar es Salaam
Ili kuhakikisha maafande wa jeshi la magereza, Tanzania Prisons, “wajelajela” wanaibuka na ushindi wa nyumbani katika mchezo wa keshokutwa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Mgambo Jkt kutoka mkoani Tanga, wadau na viongozi wa soka mkoani humo wamekutana  kujadili namna ya kuisaidia timu hiyo.
Akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu, katibu mkuu wa Prisons, Sadick Jumbe, amesema wadau wamewafariji kwa kiasi kikubwa na wameahidi kujitokeza kwa wingi kuwashangilia ili wapate ushindi wa tatu nyumbani tangu waingie ligi kuu msimu huu.
“Kitendo cha wadau kukutana na sisi ni uzalendo mkubwa sana, hii inaonesha upepo umebadilika kwa mashabiki wa jiji hili, kama hali itaendelea kuwa hivi, lazima tuwatoe kimasomaso”. Alisema Jumbe.
Katibu huyo alisema maandalizi ya mchezo huo yanakwenda vizuri, wachezaji wapo katika morali kubwa na mpaka sasa hakuna mchezaji yeyote ambaye yuko hatarini kuukosa mchezo huo muhimu.
Kufuatia Prisons kutokuwa na rekodi nzuri ya kushinda mechi za nyumbani, Jumbe  alisema kuwa sasa ni wakati wa kufuta makosa na kutumia vyema dimba la nyumbani ambalo litasheheeni mashabiki lukuki.
“Kufungwa 1-0 mechi iliyopita na vijana wa mitaa ya kishamapanda Toto Africans, ni sehemu ya mchezo, kama utakumbuka tulijifunga, kama isingetokea vile tungetoa sare, lakini mwalimu umewapanga vijana kisaikolojia ili kutumia nafasi ya nyumbani kupata ushindi”.
Wakati wajelajela wakijipanga kuwaadhibu wapinzani wao, nao Mgambo JKT kupitia kwa katibu mkuu wake, Antony Mgaya, wamesema wapo Mbeya kutafuta mzigo wa pointi tatu muhimu.
Mgaya alisema walifika mapema Mbeya ili kuzoeza hali ya hewa mkoani humo ambayo alieleza kuwa kwa sasa kuna taofauti na mikoa ya Pwani.
“Tuna kazi moja tu ya kuwafunga wapinzani wetu ingawa watakuwa mbele ya mashabiki wao wenye hamasa kubwa, lakini tumefanya mazoezi na kocha wetu Mohamed Kampira amefanya marekebisho makubwa ya kikosi chake”. Alisema Mgaya.
Tanzania Prisons wapo nafasi ya 11 wakiwa na ponti 20 kibindoni wakati Mgambo JKT wapo katika nafasi ya 9 wakijikusanyia pointi 24 kibindoni.
Ushindani wa mechi hiyo unatarajiwa kuwa mkubwa kutokana na timu zote kuwa miiongoni mwa klabu zinazohitaji kujinasua na mstari mwekundu wa kuporomoka daraja.
MGAMBO JKT

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video